• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Mwenyekiti wa Halmashauri na Mkurugenzi Mtendaji wafanya ziara ya pamoja.

Imerushwa: January 6th, 2022

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Mhe. Mussa Mwanyumbu na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Bw. Saitoti Zelothe Stephen wamefanya ziara ya  kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwenye  kila Kata na kisha  kufanya vikao na Kamati za Maendeleo za Kata (KAMAKA) kwa kila Kata kwa kata zote 21 za Halmashauri ya Handeni. Wakati wa ziara hiyo viongozi hao wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kuipatia Halmashauri ya Wilaya ya Handeni fedha kwa ajili ya ujenzi wa Miundombinu mbalimbalimbali ambayo itasaidia wananchi wa Handeni.

Mhe. Mwanyumbu na Bw. Saitoti.wameshatembea kata 5 kati ya kata 21, Kata hizo ni pamoja na Kitumbi, Mkata, Komkonga, Kabuku na Kabuku Ndani.

Mhe. Mwanyumbu amesema lengo la kufanya ziara hiyo ni kuangalia maendeleo ya miradi kwenye kila Kata na kusikiliza changamoto na kero mbalimbali zinazowakabili Kamati za Maendeleo za Kata na kuzipatia ufumbuzi ili kufanya kazi kwa ufanisi.

Mhe. Mussa Mwanyumbu amezipongeza kamati zote zilizosimamia ujenzi wa Madarasa  ambapo jumla ya kiasi cha Shilingi  bilioni mbili na milioni miambili kwa ajili ya utekelezaji wa ujenzi wa miundombinu ya vyumba vya madarasa 72 kwa shule za Sekondari na madarasa 19 ya shule shikizi 7 za Msingi kupitia Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya UVIKO-19.

Baada ya kusikiliza kero mbalimbali za Kamati za Maendeleo za Kata Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Handeni Bw. Saitoti Zelothe Stephen alitatua baadhi ya kero papohapo na kuchukuwa changamoto nyingine kwenda kuzifanyia kazi ikiwepo suala la malimbikizo ya mishahara ya watumishi  na migogoro ya ardhi..

Aidha  Bw. Saitoti ametoa maelekezo kwa Kamati za Maendeleo za Kata zote 21 za Halmashauri ya Wilaya ya Handeni kuwa Kamati zote za Maendeleo ya Kata zikae kila mwezi na zitoe tarifa za miradi kwa jamii na kutatua changamoto za wananchi, Kila Kata na  kijiji  visome taarifa za mapato na matumizi ya ofisi zao pia amepiga marufuku viongozi wa kata au vijiji kuuza ardhi bila kufuata sheria na taratibu za uuzaji wa ardhi.

 Mkurugenzi Mtendaji alihitimisha kwa kusema kuwa kila mtu kwa nafasi yake asimamie ukusanyaji wa mapato na wasiruhusu bidhaa kutoka kwenye Kijiji au Kata bila kulipia ushuru wa Halmashauri kwa kufanya hivyo mapato ya Halmashauri yataongezeka na kutoa ushauri kuwa miradi ya ujenzi inayotekelezwa na serikali ya kijiji  ikamilishwe isiishie kwenye lenta na kusubiri Serikali kuja kuimalizia ambapo itachukuwa muda mrefu husani madarasa.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Handeni Mhe. Mussa Mwanyumbu (aliyevaa shati la pink) akiwa na Mkurugenzi Mtendaji Saitoti Zelothe Stephen (aliyeva Suti) wakikagua boma la darasa la Shule ya Msingi Msilwa.

Madarasa Matano ya Shule ya Sekondari Kwaludege.

Wakikagua jengo la choo kwenye eneo ambalo wanatarajia kujenge stendi ya manasi Kabuku

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa