Naibu waziri Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala bora Mhe. Deogratius John Ndejembi amefanya kikao na watumishi wa Halmshauri ya Wilaya ya Handeni pamoja na Halmashauri ya Handeni Mji.
Baada ya kusikiliza kero na changamoto mbalimbali zinazowakabili watumishi, Mhe. Deogratius Ndejembi amesema Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan imejipambanua wazi kujadili maslahi ya watumishi ndiyo maana kwa mapenzi yake Rais alielekeza watumishi 180,000 wapandishwe madaraja kutoka idadi ya 90,000 iliyopangwa awali ya kupandisha watumishi huu ni upendo wa Rais wetu ameuonesha kwa watumishi nchi nzima.
Pia Mhe. Deogratius Ndejembi amesema kuwa serikali imetenga ajira za watumishi 34,000 ambazo zinatarajiwa kutangazwa hivi karibuni Serikali itatoa kipaumbele katika kada ya Elimu na Afya kwani Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amewekeza fedha nyingi kwenye miundombinu ya madarasa na vituo vya Afya ili kuhakikisha upungufu wa madarasa unaenda kuisha nchini.
Kwa kumalizia naibu waziri Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala bora Mhe. Deogratius John Ndejembi amewataka watumishi wafanye kazi kulingana na sheria, kanuni na taratibu za kiutumishi na amewakumbusha watumishi kwenda kuchanja chanjo ya ugonjwa wa UVIKO-19.
Akitoa salamu za Wilaya Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mhe. Siriel Mchembe amemshukuru Mhe Deogratius Ndejembi kufanya ziara kwenye wilaya ya Handeni na kuongea na watumishi wa Halmashauri zote mbili.
Pia Mkuu wa Wilaya Mhe Siriel Mchembe amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa Kuleta fedha kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha Afya Sindeni kwa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni na kituo cha Afya Malezi kilichopo Handeni Mji.
Aidha Mhe. Mchembe amesema madiwani walikuwa wanalipwa kwa fedha za mapato ya ndani lakini kwa sasa serikali kuu imebeba jukumu la kuwalipa madiwani hivyo anaishukuru serikali na kusema kuwa mapato ya ndani kwa kila Halmashauri yatatumika kwenye ujenzi wa miradi ya maendeleo.
Mhe. Deogratius John Ndejembi, Naibu waziri Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala bora akiongea na watumishi.
Mhe Siriel Mchembe akitoa salamu za Wilaya kwa Naibu waziri Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala bora.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bw. Saitoti Zelothe Stephe, akiongea kwenye kikao hiko.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmshauri ya Handeni Mji Bi. Mariamu Ukwaju Masebu akitoa tarifa ya Halmashauri yake.
Mtumishi kutoka kada ya afya akitoa changamoto zake kwa naibu waziri.
Watumishi wakimsikiliza Naibu waziri.
Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa