• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Naibu waziri wa maji awachukulia hatua wakandarasi wa mabwawa Handeni

Imerushwa: July 24th, 2018


Naibu Waziri wa maji Mh.Jumaa Aweso amewachukulia hatua wakandarasi wa mabwawa ya Manga na Mkata yaliyoko katika Kata ya Mkata Halmashauri ya Wilaya Handeni kwa kuwaweka mbaroni jana,  hii ni baada ya kutembelea mabwawa hayo kuona mwenendo wa ujenzi na wakandarasi hao kutokuonekana eneo la Bwawa la Manga kwa kujitetea kuwa wanaendelea na kazi ya ujenzi wa Bwawa la Mkata.

Akizungumza  na wananchi  wa Kata ya Mkata baada ya kutembelea mabwawa hayo amewaeleza kuwa yeye kama waziri wa maji hatakuwa kikwazo kwa wananchi kupata maji safi, salama na yakutosheleza na kwamba dhamana aliyopewa na Mh. Raisi ya kuwa naibu waziri wa maji ni ya kutetea wananchi wanyonge kupata maji safi, salama na ya kutoshelea na pia anatambua kuwa utekelezaji wa miradi ya maji inategemeana na upatikanaji wa fedha lakini maeneo mbalimbali fedha inapelekwa na watu wanatumia vibaya halafu hakuna hatua zinazochukuliwa na wananchi wanapata tabu hasa akina mama.

Aliongeza kuwa yeye ametembelea mabwawa hayo lakini hakuona kazi iliyofanyika ambayo itawafanya wananchi kupata maji na watu wanaendelea kuumia na kuteseka, Amesema haiwezekani viongozi wanakuja mara kwa mara hadi raisi katoa agizo, utekelezaji usiwepo  na sisi bado tunaendelea kubembelezana, mkandarasi  anaitwa eneo la mradi anakaidi na kudharau hivyo aliagiza Mkuu wa Polisi kuwaweka wakandarasi hao ndani ambao ni Mkurugenzi wa mradi wa kampuni ya Tansino Logistics,Mtaalamu msahuri (Don Consults) na mhandisi wa ujenzi. Amesema kuwaweka ndani wakandarasi hao siyo suluhisho kwani wananchi wa Mkata wanahitaji maji wala siyo maneno na siyo kwamba fedha hazipo ila watu wanafanya ujanja ujanja hivyo amewaahidi wananchi kulisimamia hilo na amewaagiza watu wa mamlaka ya maji Chalinze na Tanga kukutana na kumpa mrejesho wa namna gani wananchi wa Mkata wanapata maji safi kwa haraka ” haiwezekani fedha zikae kwenye benki  na watu hawana maji, hawatatuelewa”alisema.

Baada ya kutembelea mabwawa hayo  na kutoa maagizo pia aliongea na wananchi wa Kata ya Kang’ata na kuwaahidi kupata maji safi, salama nay a kutosheleza na kwamba Handeni tayari wamepewa kibali cha kuchimba visima kumi na kwa upande wa Kang’ata amewaongeza kisima kimoja katika idadi ya visiwa waliyopewa, Amemshauri  mhandisi wa maji wa Halmashauri kutumia wakala wa uchimbaji wa serikali ili wakapochimba maji sehemu wakakosa wanarudia tena kuchimba na pia hao wakala waangalie namna ya kutatua matatizo ya maji  na kwamba kutokana na changamoto ya maji serikali imetenga kiasi shilingi Bilioni 1.374 ili kutatua tatizo la maji.

Kwa upande ujenzi wa tanki la maji lililoko Kata ya Malezi Halmashauri ya mji wa Handeni Mh.Naibu Waziri amempa wiki nne mkandarasi kukamilisha mradi huo baada ya mkandarasi huyo kumweleza changamoto zilizokwamisha mradi huo kukamilika kwa wakati.

Alihitimisha kwa kuwataka wataalam kufanya kazi kwa bidii ili wananchi wapate huduma wanayopaswa kupata na kwmba wahandisi wa maji wa Halmashauri na Mkoa washirikiane kuhakikisha fedha za miradi ya maji inatumika ipasavyo na kwa wakati na pia kuhakikissha miradi inatekelezaka kwa wakati.

Naye Mbunge wa Handeni vijijini Mh.Mboni Mhita amesema kuwa changamoto ya maji Handeni limekuwa la muda  mrefu hivyo anaimani na ujio wa Mh.Naibu Waziri katika kutatua changamoto hiyo kwani akisema anatenda na kwamba baada yakutembelea mabwawa na kujionea hali halisi anaamini maamuzi mazito yatatolewa na pia watu wanaokwamisha upatikanaji wa maji Handeni wataondolewa kwenye mtandao wa maji ili wananchi wapate maji kwa haraka, Aliongeza kuwa hata kwa upande wa mradi wa HTM kuna tatizo hivyo ujio wake utatoa ufumbuzi wa namna ya kuharakisha upatikanaji wa maji Handeni.

Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh.Godwin Gondwe amemshukuru Mh. Naibu waziri wa maji kwa kuja kuona hali halisi ya maji Handeni  mwenyewe hivyo anaamini  tatizo la maji Handeni linakwisha, Amemuahidi kusimamia fedha itakayoletwa inakwenda kufanya kazi iliyokusudiwa kwani atathibiti mianya ya ubadhirifu wa fedha hizo.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bw. William Makufwe amemweleza Mh.Naibu Waziri kuwa baada ya kuona mabwawa hakujengwa kwa viwango vinavyotakiwa tulichukua hatua ya kuandika barua Wizarani ili kupata mbinu mbadala ya kutumia chanzo cha Chalinze (CHALIWASA)  ili wananchi wa Mkata wapate maji hivyo anaamini ujio wake utatatua tatizo la maji Mkata na Handeni kwa ujumla.

MWISHO.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa