• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

RAIS WA JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA AMETOA WIKI MBILI KWA WAKANDARASI WA MABWAWA YA MANGA, MKATA NA KWANDUNGWA KUWA SITE KUJENGA UPYA MABWAWA HAYO.

Imerushwa: August 6th, 2017

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.John Pombe Magufuli amewataka wakandarasi wajenzi na washauri waliojenga mabwawa ya Manga,Mkata na Kwandungwa chini ya kiwango kuwepo kwenye site ndani ya wiki 2 kuanzia leo ili kujenga mabwawa hayo kwa kiwango cha fedha ambacho tayari wamechukua cha Tsh. Bilion 2.8 au kwenda jela kuelezea namna gani watarejesha fedha hizo za watanzania .

 Amri hiyo meitoa leo alipokuwa akizungumza  na wananchi wa Handeni eneo la viwanja vya Mbwembwele Handeni Mjini akitokea Tanga kwenye uwekaji wa jiwe la Msingi wa Bomba la mafuta Linalounganisha Tanzania na Uganda.

 Rais Magufuli amesema kuwa  haiwezekani kiasi kukubwa cha fedha kama hicho kulipwa bila kuwepo kwa maji yanayowafikia wananchi.Amewataka wakandarasi kuwepo eneo la site na kujenga upya mabwawa kwa kutumia fedha zao hadi itakapofikia hatua ya certificate (cheti) ya kulipwa na Serikali Bilioni 1.2 ndipo watakapolipwa na kwamba fedha za watanzania haziendi bure na haiwezekani wananchi wa Handeni kusubiri maji kwa miaka 5 wakati fedha zao tayari zimetumika.

 Aidha amewaeleza wananchi kuwa atahakikisha tatizo la maji Handeni linatatuliwa kwasababu kuna miradi mitatu ambayo inatarajiwa kuleta matokeo chanya ikiwemo mradi wa  Bilion 2.6 unaomalizikia  utakao unganisha maji maeneo ya Manga, Mkata na Handeni, mradi wa zaidi ya Bilion 200 maji yatatolewa Pangani  na Mabwawa  hivyo kumaliza tatizo la maji .

 Amewataka wakandarasi waliopo na wajao kufanya kazi kwa weledi na  wakati ili kufikia malengo kwa wakati uliopangwa na kwamba hatakuwa tayari  kuwashikilia wakandarasi watakaokwamisha upatikanaji wa maji ya uhakika Handeni.
 “Wakandarasi mliopo na mtakaokuja mkitaka kugombana na mimi chezeni na miradi hii maji ya Handeni” amesema Rais Dk. John Magufuli.

 Kwa upande mwingine amewataka wananchi wa Handeni kuwa wavumilivu na kushirikiana vyema na watumishi wa Afya kwa sababu wanafanya kazi kubwa ya kuwahudumia wagonjwa   kulinganisha na idadi ndogo ya watumishi iliyopo, amewaeleza kuwa ajira zilisitishwa kwa muda kutokana na zoezi la uhakiki hivyo hivi punde watumishi wa Afya wataongezeka kwani ajira zimekwisha anza kutolewa. Aidha amewataka wananchi kujiunga na mifuko ya bima ya afya ili kuboresha huduma za afya na kuhakikisha wanapata huduma kwa wakati pindi wanapohitaji kuhudumiwa.

 Sambamba na hilo Rais amepiga marufuku wafugaji kulisha mifugo yao kwenye mashamba ya wakulima na kuwataka  viongozi ngazi ya Mkoa na  Wilaya kuhakikisha wanasimamia katika kutatua changamoto za wakulima na wafugaji kabla matatizo hayajakuwa makubwa  na kugeuka kero, amewataka wakulima na wafugaji  kuishi kwa amani  kwasababu  wanategemeana kwa kiasi kikubwa.

 Amewaagiza TAKUKURU kusimamia ili kubaini viongozi wanaopokea rushwa hususani kwa wafugaji ambao wanapesa  kwalengo la  kupindisha kero za wakulima na wafugaji hali inayopelekea kudumu kwa  migogoro ambayo ingeweza kutatuliwa kwa wakati.

 Amewataka wananfunzi kuhakikisha wanasoma kwa bidii na kutumia vyema fursa ya elimu bure ili kujiandaa kuwa viongozi wa baadae na kuwaeleza kwamba changamoto ya upungufu ya walimu inakwenda kutatuliwa hivi karibuni kwani ajira zimekwisha tangazwa na zilichelewa kupisha uhakiki wa watumishi waliokuwa wananufaika kinyume cha utaratibu.Amewahakikishia wanafunzi kuwa Serikali imeweka kipaumbele kwenye elimu hususani kwa watoto wa kike.

 Mwisho amepongeza wananchi wa Handeni kwa namna wanavyojishughulisha na shughuli za kiuchumi hususani  kilimo na ufugaji ambazo ni tija kwa maendeleo yaTaifa letu na kuwataka kuendelea na motisha ya kufanya kazi kwa juhudi huku wakiendelea kulinda amani na umoja uliopo ili kuendeleza Taifa. Rais pia ameahidi kumalizia barabara inayounganisha Dumila na Handeni yenye utrefu wa KM 50  kwa kiwango cha lami ili kurahisisha shughuli za kiuchumi  na usafirishaji .

 Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Joseph Pombe Magufuli amuzungumza na wannchi wa Handeni alipokuwa akimalizia ziara yake akitokea Tanga Mjini.

Image may contain: 5 people, people on stage

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Magufuli akizungumza na wananchi wa Handeni kwenye viwanja vya kwambwembwele

Image may contain: 2 people, people standing, car and outdoor

Mbunge wa Handeni Vijijini Mh. Mboni Mhita akizungumza na wananchi wa Kwachaga.

Image may contain: 3 people, people standing, tree, sky, car and outdoor

Mh. Rais John Magufuli akizungumza na wananchi wa Mkata 

  Image may contain: 29 people, people smiling, crowd and outdoor

Baadhi ya Wananchi wa Kata ya Kwachaga

Image may contain: 7 people, people smiling, people standing and suit 

Viongozi mbalimbali wakimsikiliza Mh. Rais Magufuli eneo la Manga mpakani mwa  Mkoa wa Tanga na Chalinze.

Mh. Rais Magufuli akisalimiana na wanafunzi wa Maganga sekondari kwa kuwahimiza kusoma kwa juhudi.

Mwanafunzi wa Manga Sekondari akifurahia ahadi ya Mh.Rais ya kutatua changamoto ya upungufu wa walimu hususani walimu wa sayansi.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mh. Martin Shigella akimshukuru  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutembelea mkoa wa Tanga.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa