• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

RC Shigela apongeza zoezi la ugawaji Vitambulisho Handeni

Imerushwa: January 11th, 2019


Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mh. Martin Shilega alitembelea Wilaya ya Handeni jana tarehe 10-01-2019 lengo likiwa ni kuona mwenendo wa ugawaji wa vitambulisho vya wajasiriamali na kusikiliza kero mbalimbali za wananchi ambapo alipata muda wa kuwagawia wajasiriamali zaidi ya mia moja katika miji midogo ya Segera, Kabuku na Mkata.

Akizungumza na wananchi Mh.Shigela aliwataka wajasiriamali ambao hawapo kwenye mfumo rasmi wa walipa kodi kujitokeza kwa wingi kupata vitambulisho hivyo ili kuepukana na usumbufu wa ushuru wanaotozwa kila mara kitu kinachowapelekea kutoa zaidi ya laki moja kwa mwaka badala yake wachukue vitambulisho vinavyowagarimu shilingi elfu ishirini kwa mwaka mzima.

Pia aliwapongeza wajasiriamali kwa kujitokeza kwa wingi kuchukua vitambulisho hivyo ikiwa ni kuunga mkono rai na dhamira ya Mh. Raisi ya kuhakikisha kila mjasiriamali mdogo kuwa na kitambulisho chake na kuwahakikishia watakaokosa kwa awamu hii kupata awamu ijayo na kwamba viongozi wa Wilaya wahakikishe wanawatambua na kuwaainisha wajasiriamali ambao bado hawajapata vitambulisho ili kuweka utaratibu wa wajasiriamali hao kupata vitambulisho vya wajasiriamali.

Aidha Mh. Shigela aliwataka viongozi wa Wilaya kutowatoza ushuru wowote wajasiriamali ambao wamepatiwa vitambulisho na alisema mjasiriamali hatakiwi kulipa fedha zaidi ya hiyo ya kitambulisho ambayo ni kiasi cha shilingi elfu ishirini kwa mwaka mzima “Hatutarajii kuona michango wala ushuru wala tozo wala kusukumwasukumwa”alisema.

Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh. Godwin Gondwe alimshukuru Mkuu wa Mkoa na timu yake kuja kuweka msukumo kwa wajasiriamali wa Handeni na alisema kwamba Handeni inatakribani asilimia tisini ya ugawaji wa vitambulisho, hivyo ndani ya siku mbili watakuwa wamekamilisha kugawa vitambulisho vyote elfu nne kwa Halmashauri ya Wilaya na Mji na kuwaorodhesha wale waliokosa ili waandaliwe utaratibu wa kupata.

Aliongeza kuwa wafanyabiashara wadogo wadogo wameitikia vizuri na kwamba anamshukuru Mh.Raisi kwa kuwaomboa wajasiriamali wadogo kwakuwa wakitoa elfu ishiri wanaepukana na kero za ushuru mbalimbali.

Naye Mkurugenzi Mtandaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bw. William Makufwe alisema Halmashauri ya Wilaya ya Handeni tulipewa vitambulisho elfu mbili na wameuza vitambulisho 1,677 hivyo aliahidi ndani ya siku mbili vilivyobaki vitakuwa vimeisha kutokana na mwitikio mkubwa wa wajasiriamali wanaohitaji vitambulisho.

Pia alieleza kwa masikitiko makubwa ajali ya gari la Halmashauri ambayo ilipata ajali wakati wa kwenda kugawa vitambulisho na kusababisha watumishi wanne kuumia pamoja na kupelekea upotevu wa vitambulisho 80.

Moja wa wajasiriamali Bi Saida Adamu alisema wao kama wajasiriamali wadogo wamefurahi sana na pia wanamshukuru Mh.Raisi kwa kuwatambua wajasiriamali wadogo na kuanzisha utaratibu ambao utawasaidia wao kufanya biashara yao kwa kodi nafuu kwani wamekuwa wakitozwa ushuru kila mara.



Mkuu wa wa Mkoa wa Tanga Mh. Martin Shigela wa kwanza kushoto akigawa vitambulisho kwa wajasiriamali

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa