• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

RC SHIGELLA APONGEZA UONGOZI WA WILAYA YAHANDENI KWA UHAMASISHAJI WA KILIMO CHA MUHOGO KUWATAKA MAAFISA KILIMO KUTOKA OFISINI .

Imerushwa: February 14th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mh.Martine Shigella amepongeza uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni ukiongozwa na Mkuu wa Wilaya na Mwenyekiti wa Halmashauri kwa kutekeleza vyema agizo la kilimo cha zao la  muhogo miongoni mwa wananchi wa Handeni.

Pongezi hizo zimetolewa jana alipofanya ziara ya kutembelea mashamba ya wakulima wa zao la Muhogo Kata ya Kwamsisi Halmashauri ya Wilaya ya Handeni na kusema kuwa ,2016 ilitokea hali ya upungufu wa mvua  hivyo wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi walielekezwa kuanza mchakato wa kuhakikisha Mkoa wa Tanga  unanusuriwa na kuondolewa kwenye aibu ya upungufu wa chakula.

Alisema kuwa zao la muhogo linahimili ukame, ni zao la biashara na chakula pia, hivyo amefurahi kuona  wananchi wameitikia wito kutokana na kupewa mbegu hizo bure mara baada ya viongozi kutekeleza agizo la kwenda kununua Mkuranga na  kuzigawa  kwa wananchi ili waweze kupata hamasa ya kulima.

Aliongeza kuwa dhamira ya Serikali ya awamu ya tano ni kuhakikisha wananchi wananhudumiwa na kuondokana kwa upungufu wa chakula na kuwatafutia masoko ya mazao wanayozalisha, ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa viwanda.

Mkuu wa Mkoa alisema kuwa amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Handeni kuzungumza na JKT Mgambo kwaajili ya kupata shamba la ekari 200 ili  kuzalisha mbegu za mihogo zitakazowasaidia  wananchi wa Handeni  na tayari Milioni 10 zimepatikana na zitakabidhiwa kwa Mkuu wa Wilaya kwa utekelazaji.

“ Serikali ya Tanzania imeingia makubaliano na nchi ya China ili kuwauzia muhogo ,Kwamsisi mmeonesha dhamira ya dhati kwa kulima kwa wingi zao la muhogo hadi sasa mna zaidi ya ekari 16 elfu  na ustawi ni mzuri, suala la kiwanda cha kuchakata mihogo nalibeba naenda kuwashawishi viongozi ngazi za juu waje waone mnachofanya , muendelee kufanya kazi na kuitikia wito ili kwenda sawa na kauli mbiu ya HAPA KAZI TU.” Alisema Mkuu wa Mkoa.

Aidha alimpongeza Afisa kilimo wa Kata ya Kwamsisi  Bw. Selemani Ikosi kwa kufanya kazi nzuri na kuwataka Maafisa kilimo kuacha kukaa ofisini kwani muda huo umekwisha na badala yake waende shambani kuhudumia wananchi.

“Naagiza Maafisa Kilimo wote Mkoa wa Tanga muda wa kukaa ofisini umekwisha , nendeni shambani mkahudumie wananchi na hiyo iwe ndio mwelekeo na dira ya utekelezaji wa maagizo yaliyotolewa na Mh. Rais na Waziri Mkuu ” Alisema Mkuu wa Mkoa. 

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh. Godwin Gondwe aliwahamasisha wananchi kujiandaa vyema na  kilimo cha muhogo katika msimu huu wa kilimo  unaokuja ili kuweza kuinua hali zao kiuchumi zaidi.

Ziara ya mkuu wa Mkoa wa Tanga iliambatana na mkutano wa hadhara uliofanyika Kata ya Kwamsisi kwa kusikiliza na kutatua changamoto zinazowakabili wananchi wa Kata hiyo na kutembelea shamba la SASAMUA.







Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HANDENI DC June 04, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa