• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

SERIKALI WILAYANI HANDENI IMESEMA HAITAKUWA TAYARI KUMUONA MTU YEYOTE ANAKUWA KIKWAZO KUTOA HAKI ZA MSINGI ZA WATOTO.

Imerushwa: June 20th, 2017

Serikali ya Wilaya ya Handeni imesema haitakuwa tayari  kwa mwananchi au mzazi/mlezi atakayekuwa kikwazo kwa kukosesha haki za msingi za mtoto  na wakati yupo katika nafasi ya kupata haki hizo hasa katika kipindi hiki ambacho haki zao zinatambulika ulimwenguni kote.

Hayo yamezungumzwa na Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh. Godwin Gondwe walipokuwa wanatoa msaada kwenye  kituo cha kulelea watoto wenye mahitaji maalumu na  ulemavu kilichopo  Kwamkono Wilayani Handeni.na Taasisi ya kifedha ya DTB jana.

Mkuu wa Wilaya amesema kuwa   mtoto kukosa haki ya kupata elimu,kutumikishwa katika umri mdogo, kuficha watoto walemavu kwa namna yoyote ile Serikali ya awamu ya 5 itachukua sheria, taratibu na kanuni kuhakikisha mtoto huyo anapata haki zote za msingi.

“ kitendo  cha kumsababishia mtoto kukosa haki zake za msingi kunasababisha maumivu na kuzima ndoto za mtoto huyo, sisi kama Serikali ya Handeni hatutaweza kumvumilia mtu wa namna hiyo kwani atakuwa hana tofauti na wale watu waliowatesa  na kuwauwa watoto huko Afrika Kusini. Tutahakikisha sheria, taratibu na kanuni zinachukuliwa kwa mhalifu huyo” alisema Gondwe.

Ametoa  wito kwa wazazi na walezi kuhakikisha fedha za TASAF wanazozipokea wanawanunuliwa watoto mahitaji ya shule na kuwapeleka  shule, Elimu bure wazazi wote kupeleka watoto wote wenye umri wa kuanza shule mapema kwani hakuna malipo.

“wazazi/walezi naomba tushirikiane  ili tuweze kuwafikisha  watoto kwenye ndoto zao na kuwapatia haki zao za msingi” alisema Gondwe.

Aidha ametoa rai kwenye ujenzi wa  majengo ya umma yanayojengwa kuhakikisha wanaweka miundombinu rafiki kwa walemavu ili kuwasaidia kwani ulemavu wao sio kikwazo cha kushindwa kupata haki zao za msingi.

Mwisho amewataka wadau mbalimbali kushirikiana na Serikali ili kwa umoja waweze kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili watoto  katika  kuzifikia ndoto zao.

Kwa upande mwingine Afisa Uhusiano na masoko wa taasisi ya kifedha ya Diamond Trust Bank (DTB)  Bw. Silvester Bahati amesema kuwa walipata mwaliko  kutoka kwa Mkuu wa Wilaya  na wakaona watumie fursa hiyo kwani katika kipindi hiki cha Ramadhani na maadhimisho ya mtoto wa Afrika wamekuwa wakitembelea vituo mbalimbali vilivyopo kwenye matawi yao kote Tanzania ili  kurejesha kiasi kidogo cha faida waliyoipata kwa jamii hususani kusaidia wenye uhitaji .

Aliongeza kuwa wameungana kuadhimisha siku ya mtoto wa Afrika na kituo cha Kwamkono kuonesha kuwa wao kama Taasisi wanaunga mkono jitihada za kuboresha mwenendo mzima wa maisha na makazi kwa watoto wa Afrika.

“upo karibu na jamii, hatuwezi kujiendesha bila kiuwa na jamii nyuma yetu, tunaitegemea jamii na jamii inatutegemea” alisema Silvester.

Kituo cha Kwamkono kinamilikiwa na  Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Tanga kina watoto zaidi ya 50 ambapo kilianzishwa mwaka  1963 na waanzilishi walikuwa masista wa passion for Christ kwa lengo la kushughulikia watoto walioathirika na  ugonjwa wa polio na mwaka 1973 kubadilishwa kuwa kituo cha kulelea watoto wenye mahitaji maalumu wanaoweza kufundishika.

Kituo kinajiendesha kwa miradi midogo midogo ya kulima mbogamboga, mradi wa maji unaosaidia kituo na jamii inayozunguka,vibanda vya kupangisha (fremu) na wahisani mbalimbali.

Diamond Trust Bank imetoa msaada wa vyakula na mahitaji mbalimbali ya shule kwa  watoto vyenye thamani ya milioni moja.

Baadhi ya Watoto waliopo kwenye Kituo cha Kwamkono.

Picha ya pamoja mara baada ya makabidhiano ya Zawadi.


watoto wakishangilia kupewa zawadi na Diamond Trust Bank.

Mkuu wa Wilaya Mh. Godwin Gondwe akimsaidia kuendesha kiti mmoja wa walemavu wanaotumia kiti kutembelea.


Afisa Masoko na Uhusiano Bw. Silvester Bahati wa DTB kushoto  akikbidhi zawadi kwa mkuu wa kituo hicho.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa