• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Shirika la DORCAS latatua tatizo la maji shuleni

Imerushwa: April 3rd, 2019


Shirika la kiraia linaloitwa DORCAS limekabidhi mradi wa matenki mawili ya yakuvuna maji kwa Halmashauri jana katika shule mbili za msingi ambazo ni Kweditilibe na Zavuza za Kata ya Kiva,Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Mkoani Tanga, lengo likiwa ni kuwasaidia wanafunzi kupata maji kutokana na uhaba wa maji uliopo katika maeneo hayo.

Wakati wa kupokea mradi huo Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bi.Fatuma Kalovya aliipongeza na kuishukuru shirika hilo kwa kutoa ufadhili huo ambao utatumiwa na vizazi vya sasa na vya baadaye lakini kuwahakikishia pia ufuatiliaji wa karibu wa matumizi mazuri ya mradi.

Bi Kalovya aliwaagiza viongozi wote wa vijiji na wa shule kuhakikisha wanasimamia na kutunza miundo mbinu hiyo ya maji waliyojengewa ili iweze kudumu kwa muda mrefu na wanafunzi kuendelea kunufaika.

Sambamba na hilo Kalovya amewataka viongozi wa shule hizo kuongeza gata za kupeleka maji kwenye tenki kuzuia upotevu wa maji wakati wa mvua, pia matenki kupata maji mengi yatakayotumika kwa muda mrefu kitu kitakachowafanya wanafunzi hao kupata muda wa kutosha wa kusoma badala ya kufuata maji sehemu zingine ambazo ziko mbali na shule.

Pia alitumia nafasi hiyo kuwaasa wananchi kuweka mazingira katika hali ya usafi na kuweka takataka zote katika madebe ya uchafu kuepuka magonjwa ya mlipuko kwani pamoja na shirika hilo kujenga matenki ya kuvuna maji pia limegawa madebe ya kuweka takataka.

Msimamizi wa mradi huo Bi Augusta Keiya alisema lengo hasa la mradi ni kuhakikisha pia usafi binafsi wa mtoto wa kike na hedhi salama na alisema kwa Wilaya nzima mradi umelenga kuwafikia wanafunzi elfu nne mia mbili (4200) katika shule 25 pamoja na wasichana 800 ambao hawapo shuleni. Kwa mwaka 2019 alisema watajenga matenki 6 ambapo kati ya hizo matenki matatu tayari yameshajengwa.

Keiya alisema ujenzi wa matenki hayo yenye ujazo wa lita 23000 kila moja ulianza 21/01/2019 ambapo mpaka kukamilika kila tenki liligharimu kiasi cha shilingi milioni 16.6. Ujenzi huo pia ulihusisha mafundi wa mtaani ambao walifundishwa namna ya kujenga matenki yanayotumia waya meshi na simenti pekee bila kutumia matofali au mawe kutoka shirika la SHIPO na kuwasihi mafundi hao waliofundishwa kutoa elimu hiyo kwa mafundi wengine ili wananchi waweze kupata mafundi wakutosha kwa gharama nafuu lakini pia kuongeza ajira katika jamii.

Walimu waliosoma risala akiwepo Mwl.Adamu Saidi wa shule ya msingi Kweditilibe na Mwl.Christina Mpanda wa shule msingi Zavuza walielekeza shukrani zao kwa shirika hilo kwani pamoja faida ya maji watakayopata pia walisema shirika limekuwa karibu na wanafunzi hasa wa kike kwa kutoa elimu ya usafi binafsi na hedhi salama.

Mtoto Abdalah Mokiwa kwa niaba ya wanafunzi ameishukuru sana shirika la DORCAS na SHIPO kwa kuwajengea matenki hayo kwakuwa walikuwa wanapata shida sana kupata maji ya kupikia na yakutumia chooni na alisema sasa hivi hawatakuwa na tatizo la maji kama zamani na kuahidi pia kutunza matenki hayo.

Imetolewa na kitengo cha habari

Halmashauri ya Wialaya ya Handeni.

03/04/2019

Kaimu Mkurugenzi Bi.Fatuma Kalovya akifungua maji baada ya kukabidhiwa mradi.

Fundi sanifu wa Halmashauri Bw.Omary Kipigo upande wa akikagua mradi 

Mwonekano wa matenki ya lita 23000 kila moja yaliyojengwa na shirika la DORCAS.

Msimamizi wa mradi Bi.Augusta Keiya akitoa ufafanuzi wa mradi.

Maofisa mbalimbali wa shirika la DORCAS

Wanafunzi wa shule ya Kweditilibe wakichota maji katika tenki waliyojengewa na shirika hilo


Picha ya pamoja baada ya kukabidhi mradi




Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa