• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Maadhimisho ya Siku ya wanawake Handeni

Imerushwa: March 8th, 2019

WANAWAKE WATAKIWA KUBADILI FIKRA KIUCHUMI BADALA YA KUWAZA KUNUNUA MADERA.

Halmashauri ya Wilaya ya Handeni imeadhimisha siku ya Wanawake Duniani ambayo huadhimishwa kila mwaka ifikapo tarehe 8/3 lengo likiwa ni kuwakumbusha wanawake kujikwamua kiuchumi na kujua haki zao za kisheria katika jamii. Kwa mwaka 2019 Halmashauri iliadhimisha siku hiyo katika Kata ya Kitumbi ikiwa na kauli mbiu inayosema “Badili fikra kufikia usawa wa kijinsia kwa maendeleo endelevu”.

 Maadhimisho hayo pia yaliambatana na ugawaji wa mikopo yenye jumla ya kiasi cha shilingi Milioni 15.2  kwa vikundi vitatu vya  wanawake na kikundi kimoja cha vijana.

Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo alikuwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Mh. Mustapha Beleko ambapo alisema ili mwanamke ajikwamue kiuchumi lazima atue ndoo ya maji hivyo amewahakikishia wananchi kuwa tatizo la maji lililotokana kukatwa kwa maji limeatatuliwa hivyo kuanzia leo usiku maji yataanza kutoka. Kwa upande wa Mkata alisema chazo cha Chalinze kimeanza kufanyiwa kazi na mkandarasi amepewa muda hivyo wakati wowote maji yatafika Mkata, pia alielekeza pongezi kwa Mwenyekiti wa CCM Wilaya Mh. Athumani Malunda kwa kuwa bega kwa bega kufuatilia suala la upatikanaji wa maji Handeni.

Mh. Beleko alitoa rai kwa waliochuchukua mkopo kutumia  mkopo huo kuzalisha kwani lengo la Mh. Raisi ni kuwainua kiuchumi wananchi na mkopo huo unatolewa bila riba na kwamba ili kikundi kipate mkopo mwingine lazima kirejeshe mkopo huo kwa wakati na pia itakuwa rahisi vikundi vingine kupata mkopo huo..

Aliwasihi wazazi kutokuwabagua watoto katika suala la kuwapa haki ya elimu kwamba kila mtoto lazima apate elimu hasa mtoto wa kike kwani wengi huwapeleka watoto wa kiume na kuwaacha wa kike.

Alihitimisha kwa kuwataka wananchi kujiepusha na maambukizi mapya ya UKIMWI kwakuwa kiwango cha maambukizi kimeongezeka kutoka asilimia 2.7 mwaka 2017 hadi kufikia asilimia 4 mwaka 2018 hivyo wapeane elimu kwamba UKIMWI bado upo  na waache kujiliwaza kwamba dawa za kufubaza zipo, “gharama za kununua dawa hizi ni kubwa na tunairudisha nyuma nchi kimaendeleo”alisema.

Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Mkoa wa Tanga Dr. Aisha Kigoda aliwataka wanawake kutojiweka nyuma katika shughuli za uzalishaji mali bila kuogopa changamoto na pia wasisite kufuatilia haki zao za kisheria na kwamba hakuna mafanikio bila kujishughulisha.

Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Handeni  Mh. Athumani Malunda aliwataka wanawake kutafuta fursa za kujiendeleza kiuchumi ili kuepuka unyanyasaji wa kijinsia na waache kufikiria kununua nguo badala ya kufanya kitu cha maana ambacho kitamkwamua kiuchumi hasa kujiwekeza kwenye umiliki wa ardhi.

Pia aliwasihi wazazi  kuzingatia maadili ya watoto ili kujenga kizazi kijacho chenye maadili la sivyo watapoteza kizazi kijacho chenye maadili hasa suala la mavazi na lugha staha.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bw. Simon Mdaki aliwapongeza wananchi wa Kitumbi kwa kuanzisha ujenzi wa Shule ya Sekondari na kuwasihi kuhakikisha hakuna mtoto anayebaki nyumbani hasa watoto wa kike na pia aliwasihi kujitokeza kuchangia nguvu kazi katika ujenzi wa zahanati ili kupata huduma ya afya iliyokaribu kwa akina mama hasa kupeleka watoto kliniki.

Na kwa uchaguzi ujao alisema Mdaki  wanawake wagombee nafasi mbalimbali ili iwe rahisi kusimamia haki za mwanamke katika jamii na kwamba wasikae nyuma wajiamini.

Bw. Mdaki aliwataka wananchi kujikinga na kipindupindu na kwamba viashiria vimeonekana hivyo wamama wachukue tahadhari kwani wana nafasi kubwa katika kuelimisha jamii na kuzuia kuenea kwa kipindupindu katika familia zao kwa kuwa wao  wameshika Nyanja zote za usafi katika familia

Afisa Maendeleo ya jamii Bi. Amina Waziri akisoma majina ya vikundi vya wanawake na vijana wanaopewa mikopo  alisema  ili kikundi kipewe mkopo lazima kiwe na vigezo ikiwepo usajili wa Halamashauri na uwepo wa akunti benki, kujishughulisha na uzalishaji wa viwanda vidogo, shughuli endelevu iliyokwisha anzishwa na kwa upande wa vijana alisema kikundi lazima kiwe na watu wasiozidi umri wa miaka 18- 34.

Aidha, alisema kuna vikundi viwili vinavyotarajiwa kupewa mkopo wa mashine za kuchakata mihogo vyenye thamani ya shilingi milioni 17 kila moja ikiwepo kikundi cha wanawake cha jipemoyo kilichopo Kata ya Kitumbi na kwamba mchakato wa awali umeshafanyika ikiwepo sehemu ya kuweka mashine hizo ambapo tayari serikali ya Kijiji cha Kitumbi kimewapa ekari mbili bure kwaajili ya kujenga miundo mbinu ya kuweka mashine hizo.

Mwakilishi wa wanawake Bi.Clementina Nyoni  akisoma risala alisema wanawake wapewe mikopo yenye riba nafuu ili wajikwamue kiuchumi pia aliomba viongozi wa serikali kusimamia sheria ili watoto wate katika jamii wapate elimu kwani watoto wa kike wamekuwa wakiachwa nyuma katika suala la elimu.

Katika maadhimisho hayoTaasisi na mashirika mbalimbali  zilitoa salamu za siku ya wanawake wakiwepo MNB,shirika linaloshughulika na shughuli mbalimbali za maendeleo katika jamii( TANZACARE), Shirika linaloshughulisha na afya ya jamii(DSW), wasaidizi wa kisheria(NALIDO) na TAKUKURU ambapo mwakilishi wake Bw.Mwamkamba aliwataka wanawake kutoa taarifa katika vyombo vya kisheria pale mtu anapotaka rushwa hasa ya ngono ambayo inamrudisha mwanamke nyuma kimaendeleo,  pia vikundi mbalimbali vya wanawake vilileta bidhaa zao.


Mgeni rasmi Mh. Beleko mwenye tisheti ya bluu kulia akikagua bidhaa zilizoletwa katika maadhimisho ya wanawake

Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Handeni Mh. Athumani Malunda akitoa nasaha

Mwenyekiti wa umoja wa wanawake Mkoa wa Tanga Dr. Aisha Kigoda akitoa neno  

Kaimu Mkurugenzi Bw. Mdaki akizungumza katika maadhimisho hayo

Afisa maendeleo ya jamii Bi. Amina Waziri akisoma taarifa

Burudani mbalimbali zikiendelea katika maadhimisho hayo


Mgeni rasmi Mh.Beleko wa kushoto akiwapa vyeti viongozi wa vikundi waliopewa mkopo 



Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa