• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Timu ya menejimenti ya Halmashauri ya Handeni yafanya ziara ya kukagua miradi

Imerushwa: April 8th, 2020

Timu hiyo iliyoongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Handeni Bw. William Makufwe ilifanya ziara ya kukagua mirandi mbalimbali iliyopo kwenye Halmashauri ikiwepo ujenzi wa jengo la makao makuu ya Halmashauri, ujenzi wa vyoo vya shule ya msingi Tuliani, Mradi wa kupanda miti katika kijiji cha Kwamkunga  na kiwanda cha kuchakata muhogo pamoja na kusikiliza kero za wanachi

 Mkurugenzi Mtendaji Bw. William Makufwe amesema kuwa wao kama wafanyakazi wa Hamashauri wamejiwekea utaratibu wa kutembelea miradi inayoelendelea kutekelezwa kwenye Halamshauri yake ili kuona mwenendo mzima wa maendeleo ya miradi hiyo.

 Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh. Godwin Gondwe alimpongeza Mkurugenzi mtendaji pamoja na wafanyakazi wa halmashauri ya wilaya ya Handeni kwa kutimiza agizo la Waziri Mkuu la kutoka ofisini kwenda kukagua miradi na kusikiliza kero mbalimbali za wanachi.

Pia Mkuu wa Wilaya  Mh. Godwin Gongwe amemuomba  Meneja wa wakala wa barabara za mijini na vijijini (TARURA) mkoa wa  Tanga Injinia  George Tarimo kuirekebisha barabara inayoelekea kwenye jengo la Halmashauri ya Handeni ili magari yanayopeleka vifaa vya ujenzi yaweze kupita.

Na ameagiza kuwa misaragambo yote ya kurekebisha barabara ikifanyika watu wa TARURA lazima wawepo maana wao ndiyo wataalamu wa kutoa ushauri namna ya kurekebisha barabara hizo.

Alihitimisha kwa kuwaagiza  wakala wa barabara mijini na vijijini (TARURA) Handeni,  Idara ya Ardhi, Mipango miji na idara ya misitu kukaa kikao ndani ya siku kumi ili kuandaa mpango kazi wa  makazi ya kisasa.

 Kwa upande wa Meneja wa wakala wa barabara mijini na vijijini (TARURA)  mkoa wa Tanga injinia George Tarimo amesema  atalifanyia kazi suala la kutengeneza barabara  ili magari yaweze  kupeleka vifaa kwa urahisi katika eneo la ujenzi wa jengo la makao makuu ya Halmashauri.

Naye  Katibu Tawala wa Wilaya ya Handeni Mwl. Boniphace Maiga alishauri kila barabara apewe injia mmoja ili iwe rahisi kufuatilia katika uboreshaji wa barabara hizo.

Mkurugenzi Mtendaji Bw. Wiliiam Makufwe alimueleza Mh. Mkuu wa wilaya pamoja na kamati nzima ya ulinzi na usalama ya wilaya kuwa mpaka sasa ujenzi umefikia 15% pamoja na kuwa na changamoto ya mvua na ubovu wa barabara yenye urefu wa Kilomita 1.5 kutoka barabara kuu kupitisha vifaa mpaka eneo la ujenzi wa makao makuu ya Halmshauri.

Akisikiliza na kutatua  kero za wananchi katika kijiji cha Kwamkunga Mkurugenzi Mtendaji kuhusu suala la maji amewaeleza kuwa wataalamu wa maji watakwenda kufanaya tathimini ya mabomba na gharama na kuona namna ya kufikisha maji kijijini hapo, na kwa upande wa umeme amesema tathimini imeshafanyika tayari  mradi wa umeme utafika kwamkunga.

Kuhusu kero ya zahanati Makufwe amewaagiza wanakijiji hao kuwa mpaka mwezi wa tisa wawe  wamefyatua matofali ya kuchoma elfu kumi na tano (15,000) ili ujenzi wa zahanati uanze mara moja kijijini hapo halafu Halmashsuri inakwenda kumalizia.  

 Wakati wakikagua shamba la miti la ekari mia moja (100) lililopo kijiji cha Kwamkunga Afisa misitu wa Halmashauri ya wilaya ya Handeni Bw. Elinihaki Hashim Mdee alisema wamepata msaada wa fedha kutoka  mfuko wa Misitu Tanzania kiasi cha milioni 93 kwaajili ya kuboresha misitu na ekari 50 za shamba zimeshasafishwa tayari kwa kupanda miti.

Kwaniaba ya wananchi wa kijiji cha Kwamkunga, Kata wa Kwankonje Diwani wa kata hiyo Mh.Jonathan Maturu alishukuru timu ya menejimenti ya Halmashauri ya Handeni kwa kufika kijijini hapo na kusikiliza kero za wananchi wa Kwamkunga na kupata majibu ya kuridhisha, pia alisema wananchi wameukubali na kuupokea mradi mkubwa wa miti na kuahidi kutoa ushirikaino.

 Mkuu wa wilaya ya Handeni Mh. Godwin Gondwe wa kwanza kulia akipokea taarifa ya ujenzi wa jengo la makao makuu ya Halmashauri kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji Bw. Wiliiam Makufwe wa kwanza kushoto.

Mh. Godwin Gondwe mwenyemiwani kulia akimuagiza meneja wa wakala wa barabara mijini na vijijini (TARURA) wa Halamashauri ya Handeni wa pili kushoto kurekebisha barabara inayoanzia sheli ya mogas kuelekea Mhalango ziliko ofisi za Halmashauri. 

Katibu tawala Wilaya ya Handeni Mwl. Boniphace Maiga katikati akitoa maelekezo kwa wataalamu wa barabara katika ziara hiyo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halamshauri ya Handeni Bw. William Makufwe aliyenyanyua mkono, akitoa maelekezo katika ujenzi wa makao makuu ya Halmashauri.

Bw. William Makufwe watatu kulia akiongea na wafanyakazi wa shamba la miti Kwamkunga.

 Afisa utumishi Bi. Fatuma Kalovya  katikati akifafanua jambo wakati wa ziara hiyo.

 Wafanyakazi wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni wakiwa eneo la ujenzi wamakao makuu ya Halmashauri. 

Jengo la makao makuu ya Halamashauri ya Wilaya ya Handeni likiendelea kujengwa. 

 Shughuli za uchimbaji wa mashimo zikiendelea kwenye shamba la miti Kwamkunga.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa