• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

UKIMWI UPO! WANANCH JIKINGENI NA MAAMBUKIZI YA UKIMWI KWA USTAWI WA FAMILIA NA TAIFA KWA UJUMLA.

Imerushwa: December 1st, 2017


 Wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni wametakiwa kuchukua hatua stahiki ili kujikinga na maambukizi ya virusi vya ukimwi kwani UKIMWI upo  na maambukizi bado yapo.

 Rai hiyo imetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Hamlamashuri ya wilaya ya Handeni William Makufwe ambaye ndiye mgeni rasmi  kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya, kwenye maadhimisho ya siku ya Ukimwi duniani yenye kauli mbiu  ya “ Changia  mfuko wa udhamini wa ukimwi,okoa maisha, Tanzania bila ukimwi inawezekana”.


 Makufwe alisema maadhimisho ya siku ya ukimwi duniani yanatoa nafasi kwa wananchi na jamii kujitathmini, kujipima na kujitafakari katika kujua tabia na mienendo katika kujikinga na janga zima la ukimwi.

 Aliongeza Kuwa UKIMWI ni tatizo kubwa ulimwenguni hususani kwa nchi zinazoendelea, na kwamba Handeni kama maeneo mengine ya Tanzania wanakila sababu ya kutafakari na kutathmini kuhusu athari za ukimwi na namna ya kupambana na maambukizi mapya.

 Makufwe amesema Serikali inajitahidi kupambana na janga la Ukimwi kwakua athari zake ni kubwa ikiwemo kuongezeka kwa watoto yatima,kupoteza nguvu kazi hatimaye kuongezeka kwa umasikini ngazi ya familia hadi taifa hivyo ni muhimu kuchukua hatua stahiki kujikinga na maambukizi mapya. 

 Aidha ametoa wito kwa wananchi kujitokeza katika upimaji wa afya zao mara kwa mara, kupinga ndoa za utotoni, kufanya kazi kwa bidii kuepuka vishawishi  na kuhakikisha wazazi na walezi wanawalea watoto na vijana wao katika maadili yaliyomema  yatakayowasaidia  kujiepusha na maambukizi ya Ukimwi.

 Kwa upande wake Makamu mwenyekiti wa Halmashauri na Mwenyekiti wa Kamati ya Ukiwmi Mh. Abdallah Pendeza amesema ukimwi upo na maambukizi yanaongezeka  ni vyema kwa kutumia maadhimisho haya  hatua ikachukuliwa.

 Alizitaka kamati za ukimwi ngazi ya Kata na Vijiji kuhakikisha zinafanya kazi ya kuelimisha wananchi kuacha ngono zembe na visababishi vingine vinavyosababisha maambukizi ya virusi vya Ukimwi.
 Maadhimisho ya Ukimwi Halmashauri ya Wilaya ya Handeni  yamefanyika katika  shule ya Msingi Magamba kata ya kwaluguru na kushiriki kwa vikundi mbalimbali  vya burudani.


Image may contain: 9 people, crowd and outdoor

Image may contain: 7 people, people sitting and flower

Image may contain: 16 people, people smiling, crowd and outdoor 


Image may contain: 6 people, people standing, crowd and outdoor





Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa