• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

UONGOZI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA HANDENI UMEKABIDHI PIKIPIKI 2 KWA WATENDAJI WA KATA MBILI KAMA MOTISHA.

Imerushwa: August 31st, 2017

Uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni  umetoa pikipiki mbili zenye thamani ya Shilingi Milioni 4 na laki 5 kwa Watendaji wa Kata za Kwasunga na Kang’ata ikiwa ni maagizo  ya Baraza ya  kutoa motisha kwa Watendaji hasa wanaofanya vizuri  kukusanya  mapato na waliopo kwenye mazingira magumu ya kukusanya Mapato . 

 Motisha hiyo imetolewa leo mara baada ya kumalizika kwa Baraza la Madiwani la kufunga mwaka lililofanyika kwenye ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni.

 Akikabidhi pikipiki hizo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Mh. Ramadhani Diliwa  amesema kuwa dhamira yao kama Baraza ni kusaidia na kusimamia shughuli za maendeleo na suala zima la ukusanyaji wa mapato katika   kata zote.


 Ameongeza kuwa Madiwani wanafahamu Halmashauri inakipato kidogo , wangengeweza kugawa pikipiki  kwa kata zote 21, lakini  ni bora kuanza kuliko kuacha kabisa hivyo lazima  Madiwani wote waridhie kama walivyopitisha, maana kwa popote  zitakapoenda ni Halmashauri hiihii ya Handeni na sio mwisho mapato yatakapoongezeka pikipiki zitaendeleakununuliwa ili kata zote 21 ziweze kupata.

 Aidha amewata Watendajji kuacha kuchukulia kuwa ni mali ya Serikali na kushindwa kutunza, na kwamba Watendaji wanaokabidhiwa  wazitunze kama ambavyo wangeweza kutunza za kwao ili ziweze kudumu kwa muda murefu.

 “Watendaji nawaeleza pikipiki hizi zisiwe na mikono mingi, muache kufanyia kazi ambazo hazihusiani na malengo yaliyokusudiwa, kama kupakiza mbao, mikaa,magogo na kadhalika msizichoshe mapema, kafanyieni kazi ya Halmashauri ili zidumu kwa muda mrefu na wengine waje waige kutoka kwenu” Amesema Mh. Diliwa.

 Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Bw. William Makufwe amesema kuwa wametimiza  maagizo waliyopewa na Baraza ya kutoa motisha kwa watendaji watakaofanya vizuri kwenye kukusanya mapato na walio na waliopo katika mazingira magumu hususani pembezoni ambao wanapata chanamoto kubwa ya kukusanya mapato.

 Aidha ameeleza kuwa pikipiki hizo ni mali ya Halmashauri na Kata huika na sio mali ya Mtendaji Kata,lengo ni kusaidia katika shughuli za kukusanya mapato na shughuli nyingine za kiutawala hivyo matumizi Binafsi Hayaruhusiwi. 

 Ameongeza kuwa motisha zitaendelea kutolewa kadri fedha zitakapopatikana na Kwamba lengo la Halmashauri ni kuhakikisha Watendaji wote wanapata vitendea kazi ambavyo vitasaidia kuongeza ufanisi wa kazi wakati wowote.

 Kwaupande wao watendaji wa Kata za Kwasunga na Kang’ata wamepokea kwa furaha vitendea kazi hivyo na kusema kwamba zitawasaidia kufanya kazi kwa weledi na mtawanyiko mkubwa kwenye maeneo yao hali ambayo itapunguza changamoto za ufuatiliaji wa shughuli za mapato na kiutawala katika maeneo yao. Wametoa rai kwa Watendaji wenzao kuongeza juhudi katika kutenda kazi kwa weledi na uadilifu ili kufikia malengo ya Halmashauri.


Image may contain: 2 people, people sitting, motorcycle and outdoor

Mtendaji Kata ya Kwasunga kushoto na Mtendaji Kata ya Kang'ata kulia wakiwa na pikipiki zao mara baada ya kukabidhiwa.

Image may contain: motorcycle and outdoor

Pikipiki zilizokabidhiwa

Image may contain: 9 people, people standing 

Mh.Diwani Kata ya Kabuku ndani aliyeketi kwenye pikipiki kuonyesha wameziokea kwa furaha

Image may contain: 10 people, people smiling, people standing

Waheshimiwa madiwani wakipokea pikipiki kwa furaha

  Image may contain: 10 people, people smiling, people standing

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wiaya ya Handeni Bw. William Makufwe mwenye joho la Blue akizungumza na Madiwani.










Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa