• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

RC SHIGELLA AKABIDHI VIFAA VYA MATIBABU ZAHANATI YA KOMKONGA NA KUWATAKA WATUMISHI KUFUATA MAADILI YA KAZI.

Imerushwa: February 14th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mh. Martine Shigella amewataka wafanyakazi wa Zahanati ya Komkonga kutumia vifaa vilivyonunuliwa kwa fedha iliyotolewa na Raisi wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mh. John Pombe Magufuli tarehe 3/8/2017 alipofanya ziara Mkoani Tanga, kwa kuzingatia maadili ya kazi na kuhakikisha wananchi wanahudumiwa kwa upendo na lugha nzuri bila  kuwepo kwa dalili za udokozi na wizi wowote .

Rai hiyo ameitoa jana alipokuwa akikabidhi vifaa vilivyonunuliwa kwaajili ya kuboresha matibabu ya wananchi wa Kata ya Komkonga na kusema kuwa fedha alizoziahidi Rais  kiasi cha Milioni 10 zilitolewa mapema Kabla ya kuondoka mara baada ya kumaliza ziara yake.

Aliongeza kuwa kwasababu zilikuwa ni fedha za umma hivyo taratibu za manunuzi zilipaswa kufuatwa ambapo Halmashauri ya Wilaya ilifuata kwa kuagiza vifaa hivyo kwenye  bohari kubwa ya dawa na vifaa tiba ya MSD(Medical Stores Department),ambapo baadhi ya vifaa vilipatikana na vingine ilibidi viagizwe kutoka sehemu nyingine kutokana na MSD kutojitosheleza kwa kuwa na vifaa vyote.

Alisema kuwa manunuzi yamekamilika na vifaa vyote vilivyohitajika vimekamilika ndiyo maana vimekabidhiwa na Kumshukuru  Rais kwa upendo wake aliouonesha kwa wananchi wa Tanga hususani Handeni Kata ya Komkonga, kwasababu upatikanaji wa vifaa hivyo utawasaidia kuondokana na tatizo lililokuwa sugu katika Zahanati ambako ndipo huduma za matibabu zinatolewa.

Aidha alipongeza uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni na wananchi wa Kata ya Komkonga kwa namna ambavyo wamejitoa kwaajili ya kujenga maabara ndogo inayotarajiwa kumalizika baada ya siku nne, itakayokuwa inatumika kuhifadhia vifaa  kwani kwa kufanya hivyo kutasaidia usalama wa uhakika.

 Wakati huhohuo amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni kupitia taratibu za madaktari kuhakikisha ndani ya mwezi mmoja anafuatilia na kujiridhisha juu ya  tuhuma zinazomkabili Daktari wa Zahanati ya Komkonga, zilizotolewa dhidi yake na wananchi ili kama kuna ukweli hatua zichukuliwe na kupewa onyo, na kama akiendelea afukuzwe kazi sababu Serikali haiwezi kumvumilia mtu ambaye anajifanya ni Mungu mtu.

“Marufuku kwa mtumishi yeyote wa umma kumhudumia mwananchi kwa lugha ambayo haina staha,yeyote atakayebainika kukiuka agizo hili aripotiwe kwa Viongozi wa Wilaya na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ili hatua zitachukuliwa, Kila mtu anahitaji kuheshimiwa na kuthaminiwa utu wake” alisema Mkuu wa Mkoa.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh. Godwin Gondwe alishukuru kwa mapokezi ya vifaa hivyo na kuahidi kushirikiana na Ungozi wa Halmashauri katika kuhakikisha malengo yaliyokusudiwa yanafikiwa.

Akisoma taarifa ya vifaa vilivyonunuliwa Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Dk.Credeanus Mgimba alisema vifaa hivyo ni pamoja na Vitendanishi vya kupimia taiphodi, mashine ya kuchanganyia sampuli mbalimbali, hadubini, mashine ya kupima wingi wa damu pamoja na vitendanishi vyake ambavyo vimepatikana kupitia fedha za Wizara ya Afya, mashine ya kupimia magonjwa yatokanayo na mkojo na vitendanishi vya kupimia magonjwa ya mkojo, ambapo vimegharimu Tsh.5,296,300/= na kubakiwa na bakaa la Tsh.4,370,000/= iliyopo MSD Tanga itakayokuwa inatumika kuagizia vitendanishi ambavyo vinaukomo kwa kuletwa kwa awamu sababu matumizi yake ni ya taratibu.

Mkurugenzi Mtendaji Bw.William Makufwe aliyevaa shati la draft nyeusi na Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh. Godwin Gondwe aliyevaa shati la draft nyeupe wakisikiliza wananchi wa Komkonga namna walivyohamasika kushiriki nguvu kazi ya ujenzi wa maabara ndogo ya Zahanati yao.

Jengo la maabara ndogo likiwa linaendelea kwa ujenzi wakati Halmashuri ya Wilaya ya Handeni imechangia kiasi cha Milioni 3.5 kwajili ya umaliziaji na wananchi wa komkonga wakishiriki nguvu kazi na kuleta baadhi ya vifaa kama michanga na kokoto.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya HANDENI Bw. William Makufwe akieleza namna alivyoshirikiana na kamati ya Zahanati na viongozi wa Kata katika kuhakikisha wanapata maabara ndogo ya kuhifadhia vifaa.

Viongozi wakisikiliza kwa makini taarifa ya vifaa vilivyonunuliwa kwaaajili ya kuboresha huduma za matibabu kwenye Zahanati ya Komkonga.

Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Dk. Credeanus Mgimba akisoma taarifa ya vifaa vilivyonunuliwa.

Mkurugenzi Mtendaji Bw. William Makufwe akisaidiana na mganga mkuu katikati na mKuu wa Mkoa kutoa hadubini tayari kwa kuikabidhi kwa viongozi wa Komkonga.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Mh. Ramadhani Diliwa akishukuru kwa kuletewa vifaa vitakavyosaidia kuboresha huduma ya Afya kwa wananchi wa Komkonga na kupunguza adha ya kufata hudduma hizo maeneo ya Mkata na Handeni.

Mkuuwa Mkoa wa Tanga Mh. Martine Shigella akionesha hadubini kwa wananchi kwa lengo la kuboresha afya.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Komkonga Bw.Omary Mngazija akishangilia kupokea hadubini ikiwa ni moja ya kifaa alichokabidhiwa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mh. Martine Shigella mwenye suti ya kijivu  kwaajili ya kuboresha huduma za Zahanati ya Komkonga.

Baadhi ya Wananchi wa Komkonga.

Mkuuwa Mkoa wa Tanga Mh.Martine Shigela akizungumza na watumishi na wananchi wa Komkonga juu ya utunzaji wa vifaa hivyo na kupongeza uongozi wa Halmashuri kwa ujenzi wa maabara ndogo.


Mkuu wa Mkao wa Tanga Mh.Martin Shigella akikabidhi hadumini kwa mwenyekiti wa Kijiji cha Komkonga Bw.Omry Mngazija.

Katibu Tawala Mkoa Bi.Zena Saidi akisalimia wananchi wa Kata ya Komkonga.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa