• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni wafanyiwa mafunzo ya TASAF awamu ya tatu

Imerushwa: May 9th, 2018


Viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni  wamefanyiwa mafunzo ya siku tatu lengo likiwa ni kujengewa uelewa wa mpango wa kunusuru Kaya maskini (TASAF awamu ya tatu) yaliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya kuanzia tarehe 07/05 hadi 09/05 ambapo mafunzo hayo yalifunguliwa na mgeni rasmi Bw.William Makufwe ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni.

 Mafunzo hayo yalifanyika kwa makundi ambapo siku ya kwanza yalifanyika kwa  wakuu wa idara,vitengo na sehemu, siku ya pili yalifanyika kwa waheshimiwa madiwani , Mbunge na viongozi wa CCM Wilaya na siku ya tatu yalifanyika kwa  watalaamu wa Halmashauri makao makuu na  ngazi na Kata.

Akifungua mafunzo hayo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bw.William Makufwe amewaeleza Wataalamu kuwa lengo la TASAF kuja kwenye jamii zetu ni kuona namna ya kuwezesha Kaya maskini kuweka akiba na kubuni miradi mbalimbali ya mtu binafsi au ya kikundi ili kutoka kwenye Kaya maskini kwenda kwenye Kaya zenye unafuu na kwamba ifike hatua Kaya zisiwe maskini daima ziwe Kaya yenye uwezo wa kukidhi mahitaji yao .

Ameongeza kuwa TASAF watabaki kuwa wawezeshaji lakini shughuli zote zinaratibiwa na kusimamiwa na viongozi wa Halmashauri hivyo kila mtu anapaswa kujua  nini anatakiwa kufanya kwa nafasi yake katika kuhakikisha kuwa mpango huu unafanikiwa ndiyo maana kuna wataalamu wa kila taaluma katika mafunzo haya ya kujengewa uwezo wa mpango huu wa kusuru Kaya Maskini yaani TASAF awamu ya tatu “Kila moja ajue anawajibu  katika kufanikisha mpango huu” alisema.

Alihitimisha kwa kuwashukuru viongozi wa TASAF makao makuu kwa kuleta mradi huo katika Halmashauri ya Wilaya ya Handeni kwani kwa Mkoa wa Tanga Halmashauri ya Wilaya ya Handeni ndiyo Halmashuri pekee iliyopata mradi huo.

Naye Mratibu wa mafunzo ya kujenga uelewa kuhusu kuweka akiba na kukuza uchumi wa Kaya kutoka TASAF makao makuu  Bw.Hamisi Kikwape amewaeleza wawezeshwaji kuwa lengo la mafunzo hasa ni kukumbushana na tangu TASAF ianze kwa kitu chochote ambacho kinakianzishwa lazima viongozi wafanyiwe uelewa wa namna ya kuteleza shughuli husika ili utekelezaji unapofanyika kila moja anafahamu.

 Amesema dhana ya TASAF awamu ya tatu ina vitengo vinne ambavyo ni uhawishaji fedha au ugawaji fedha kwa kiasi kilichokubaliwa katika Kaya  ambayo inahusisha ruzuku ya masharti kama fedha za shule na matibabu, ajira za muda ambayo itampatia mlengwa kipato ambapo ajira ya muda imetekelezwa katika Halmashauri 44 nchi nzima. Kitengo kingine ni kuweka akiba na kukuza uchumi wa Kaya ambayo ina lengo la kuandaa mazingira ya Kaya maskini kuweka akiba na kubuni shughuli za kiuchumi ambazo zitawasaidia kuwa na hali nzuri za kiuchumi na kujitegemea hata baada ya TASAF kuondoka au baada ya walengwa kutoka kwenye mpango.

Sehemu ya tatu ni kuboresha miundo mbinu ambapo hii inatokea pale walengwa wanashindwa kutekeleza ruzuku ya masharti kwamba walengwa wanashindwa kupata elimu au matibabu kutokana na uhaba wa madarasa au hospitali hivyo jamii husika inatengeneza maombi na kutuma TASAF kwa kupitia hatua zote zinazotakiwa kupita kwaajili ya kupata fedha za kutekeleza ujenzi wa miundo mbinu hiyo. Sehemu ya mwisho ni kujenga uwezo katika mikakati mbalimbali ya kutekeleza mradi kuanzia ngazi ya Taifa hadi kijiji na kwamba walengwa wanatakiwa kueleweshwa namna ya kutumia fedha,biashara  ya kufanya,faida itakayotokana na mradi,kitu gani walengwa hawapaswi kufanya,nini wanapaswa kufanya na namna gani ya kufanya katika kila hatua ya mradi husika na pia kufanya ufuatiliaji wa jinsi shughuli zilivyofanyika.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa