• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni wamefanya kikao na kamati ya usimamizi wa ujenzi wa Kituo cha Afya.

Imerushwa: April 20th, 2018


Viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni  wamefanya kikao leo na kamati ya usimamizi wa ujenzi wa kituo cha Afya  kilichopo katika Kata ya Kabuku ambacho kinajengwa kwa fedha ya (Force occount) kiasi cha shilingi milioni mia nne,kamati hizo ni  kamati ya Manunuzi,Kamati ya ujenzi na uhamasishaji na kamati ya mapokezi na ulinzi. Majengo yanayojengwa ni maabara, chumba cha upasuaji, wodi ya wazazi, nyumba ya mganga, chumba cha kufulia na chumba cha kuhifadhia maiti.

Katika kikao hicho Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni  Bw.Ramadhani Diliwa amewaeleza wanakamati kuwa washirikiane katika kazi ya kufanikisha mradi kukamilika kwa wakati kwani tumepata fursa hivyo hatuna budi kutumia vizuri ili kukuza hadhi ya mji wetu wa Kabuku na kwamba tusiingize umimi katika kazi hii kila mtu afanye kazi kwa nafasi yake.

Aidha amewahimiza viongozi wa Kata kuwa pale inapohitajika  nguvu za wananchi  ifanyike hivyo kwani ndivyo mradi unavyotaka kwa hiyo wananchi wahamasishwe ili wajitokeze kwa wingi na kwamba mafanikio yetu ni mradi kukamilika na kuhudumia wananchi . Ameongeza kwamba mradi siyo wa mtu binafsi bali ni wa Kabuku yote na utawasaidia wananchi wote, alisema”tutokeni tukafanye kazi”.

Pia Mkurugenzi  Mtendaji  wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bw.William Makufwe amezitaka kamati hizo kutoa taarifa ya matumizi kila baada ya wiki mbili kwenye kamati ya Kata na pia kwenye mkutano wa hadhara ili wananchi wajue maendeleo ya mradi  na kwamba kamati ya manunuzi na kamati ya mapokezi zikae kila baada ya siku tatu ili waandae taarifa kwa pamoja kwaajili ya kusomwa kwenye vikao hivyo. Aidha amesisitiza leja ya kujaza vifaa kuwepo mahali ambapo vifaa ya ujenzi vinahifadhiwa kwaajili ya kujaza idadi ya vifaa vinavyoletwa na vinavyotumika na pia kuhakikisha leja hizo zinajazwa kwa wakati .

Pia amewahimiza viongozi wa Kata kuleta watu wasiopungua kumi na tani(15) kwa kila kijiji kila siku kuongeza nguvu kazi ya kutosha  ili mradi ukamilike kwa wakati. Aliongeza kuwa  kamati zifanye kazi zao bila kuingiliana majukumu ili kila moja iweze kufanya kazi kwa uhuru.Lakini pia aliwataka wanakamati kutomvumilia fundi ambaye hatafanya kazi kwa weledi na kwa wakati na kwamba inapotokea hali kama hiyo apewe onyo na akiendelea hivyo aondolewe mwingine awekwe ili mradi ukamilike kwa wakati na kuhudumia wananchi hasa akina mama.

MWISHO

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa