• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

VIONGOZI WANAOTUMIA VIBAYA FEDHA ZA MIRADI ZINAZOLETWA NA SERIKALI KUCHUKULIWA HATUA.

Imerushwa: November 22nd, 2017


 Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh.Godwin Gondwe ameagiza kuchukuliwa hatua za kisheria kwa viongozi wote wabadhilifu wa fedha zinazotolewa na serikali kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu kwani wanakwamisha utekelezaji wa miradi hiyo.

 Mkuu wa  Wilaya ameyazungumza hayo kwenye mkutano wa hadhara uliokuwa na lengo la kuhamasisha wananchi kushiriki kwa kujitolea katika ujenzi wa miundombinu ya madarasa  iliyopo kwenye maeneo yao kwa maenedeleo yao na taifa kwa ujumla.


 Mh. Gondwe alisema kuwa Ofisi ya Mkurugenzi imebaini baadhi ya viongozi kutumia vibaya fedha zilizotolewa kwaajili ya ujenzi wa miundombinu ya madarasa katika Shule ya Sekondari ya Kiva na kumwagiza Mkurugenzi Mtendaji kumsimamisha kazi Mkuu wa Shule hiyo kwa kuzidisha bei ya manunuzi ya vifaa vya ujenzi wa madarasa kulingana na bei iliyopo sokoni.

 “Mwalimu huyu asimame kazi  kwanza na mkaguzi wa ndani natoa  siku 7 awe amemaliza kuchunguza taratibu za manunuzi  na yeyote atakayebainika kuhusika kwa namna yeyote hatua za kinidhamu zitachukuliwa, fedha ya Serikali haichezewi” alisema Gondwe.

 Aliongeza kuwa maendeleo hayataletwa na wananchi kutoka nje ya Handeni na kuwataka viongozi na wananchi kuwa na nidhamu na fedha zinazoletwa kwaajili ya kuboresha shule kwa manufaa ya watoto wao, na kwamba wao kama wananchi wanao wajibu wa kushiriki kwenye ujenzi wa  miundombinu badala ya kuachia fedha inayoletwa na Serikali kufanya kazi pekee.

 Aliongeza kuwa viongozi lazima wasimamie matumizi ya fedha na kuwashirikisha wananchi kwa kila fedha inayoingia na matumizi yake ili kuweka uwazi kwa wananchi na kujua kinachoendelea ili kuwapa motisha ya kuendelea kujitolea kwenye ujenzi wa miundombinu.

 Aidha amewataka kupanga ratiba ya ushiriki wa Kila kitongoji kwenda kusaidia mafundi ili miradi inayojengwa iweze kuisha kwa wakati na kusaidia kupunguza gharama ili fedha zitakazobakia zitumike kwenye ujenzi wa miundombinu mingine kama maabara, nyumba za walimu na zahanati.

 Kwaupande wake  Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bw. William Makufwe amesema kuwa shule ya Kiva Sekondari na shule ya Msingi Kwechigwe fedha zimeletewa na Serikali Kuu  kiasi cha Milioni 66 kwaajili ya ujenzi wa madarasa 3 na matundu 6 ya vyoo.

 Aliongeza kuwa ili kuboresha mazingira  matundu ya vyoo yameongezwa na kuwa 18 na kuongeza ofisi moja ya waalimu kwa kila shule ili kuboresha zaidi miundombinu ya kujifunzia na kufundishia, Hivyo hatutakua tayari kumvumilia mtumishi anayekwenda kinyume na taratibu.

 Hata hivyo fedha hizo  zinatumia utaratibu wa  ushirikishwaji wa wananchi na kutoa nafasi ya ajira kwa vijana ambapo  ametafutwa fundi mtaalamu na uongozi wa shule unanunua vifaa vya ujenzi.


Image may contain: 1 person, shoes, tree, child and outdoor

Image may contain: 3 people, people standing and outdoor

Image may contain: one or more people, people standing, plant and outdoor 

Image may contain: 6 people, people sitting and outdoor 


Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa