• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

VIONGOZI WILAYANI HANDENI WAMETAKIWA KUSIMAMIA MIRADI NA MIUNDOMBINU ILIYOPO

Imerushwa: September 29th, 2017

Mkimbiza Mwenge wa uhuru kitaifa Ndg. Amour Hamad Amour amewataka viongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Handeni kusimamia na kutunza  kwa karibu miundombinu iliyopo .

 Amezungumza hayo wakati alipokuwa anatembelea na kuzindua miradi ya Mwenge wa Uhuru Halmashauri ya Wilaya ya Handeni tarehe 28/9/2017,amesema kuwa Serikali inatumi fedha nyingi, Wananchi wamejitolea kuchangia gharama kubwa  hivyo kuharibika kwa miundombinu hiyo ni sawa na kutoitendea haki Serikali na nguvu kubwa Wananchi waliojitolea kuchangia kwenye miradi ya maendeleo.

 Ndg.Amour amesema kuwa ili kutekeleza uchumi wa viwanda nchini kwetu tunahitaji wasomi wanasayansi, wakulima  bora  kwa kuzingatia  utunzaji bora wa mazao yetu na kuongezea thamani bidhaa zetu, Afya zilizoimarika kwa wananchi wote, viwanda vidogovidogo na kwamba hakuna budi kuhakikisha miundombinu inatunzwa na kuimrisha afya zetu. 

 Amepongeza pia Halmashauri ya Wilaya ya Handeni kwa namna ambavyo imetekeleza maagizo ya Serikali ya Awamu ya Tano kwa kufungua  Bohari ndogo ya Dawa na ujenzi wa Maabara bora  za kisayansi kwa shule za Sekondari zitakazowezesha kuwa nawahitimu wazuri wa Sayansi ili kufikia malengo ya kuwa Tanzania yenye uchumi wa Viwanda.

 Alipokuwa anazindua Bohario ndogo ya Dawa  Ndg. Amour ametoa rai kwa wananchi kuacha kutumia dawa kama chakula bila kufuata taratibu za vipimo na ushauri kutoka kwa madaktari na kwamba wanapohisi dalili za kuumwa wafike Hospitali kupata maekezo juu ya matumizi sahihi ya dawa husika.

 Aidha  Amewataka wananchi kuondoa dhana kwamba dawa zinazotengenezwa nje ya Nchi ni bora zaidi kuliko zile zinazotengenezwa Tanzania huku akitolea mfano wa dawa aina ya panadol inayotengenezwa nchini Kenya.

 Amewatak wafanyakazi kuhakikisha wanatoa huduma bora kwa wananchi wote bila kujali tofauti na kuacha kufanya kazi kwa mazoea ili kuendelea kulijenga Taifa letu kwa kupiga vita Rushwa, magonjwa ya Ukimwi na Malaria, Dawa za kulevya na kutoa elimu thabiti kwa wananchi, ikiwa ni pamoja na kuelimisha na kuhamasisha wananchi kushiriki kikamilifu kuchangia shughuli za kimaendelo kwenye maeneo yao.

 Amour amepongeza miradi yote na kutuma salamu za pongezi kwa Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh. Godwin Gondwe ambaye alikuwa na majukumu mengine na nafasi yake kukaimiwa na Mkuu wa Wilaya ya  Korogwe Eng. Robert Gabriel kwa namna ambavyo amejipanga kuhakikisha maendeleo yanapatikana Wilayani Handeni na juhudi kubwa anazofanya.

 Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh. Robert Gabriel ameahidi kufikisha salamu hizo za pongezi na kuhakikisha maelekezo yote yaliyotolewa na Mkimbiza mwenge Kitaifa Ndg.Amour Hamad Amour yanafanyiwa kazi kwa ukamilifu wake.

 Mwaka 2017 Mwenge wa Uhuru umepokelewa na kukimbizwa kwa kilomita 128 katika Halmashauri ya Wilaya ya Handeni na umepitia Miradi ya Maendeleo 8 yenye thamani ya Tshs 2,030,619,096/=  katika sekta za Elimu, Afya, Kilimo, Maji na Ujasiriamali. Halmashauri imechangia Tsh.106,366,735/=, Serikali Kuu Tsh.568,412,342/=, Nguvu za wananchi  Tsh.383,745,607 na wadau wa maendeleo Tsh. 972,094,412/= Kati ya Miradi hiyo 5 imezinduliwa, 2 imewekewa mawe ya msingi, 1 umetembelewa na kukabidhiwa cheti cha utambulisho.

 Halmashauri ya Wilaya ya Handeni imekimbiza Mwenge wa Uhuru kuanzia tarehe 28-29/9/2017 na kuukabidhi Wilayani Pangani Mkoani Tanga.

Image may contain: 3 people, people standing, sky and outdoor

Mkurugenzi wa Halmashauri ya MJI Handeni Kenneth Haule akiwa tayari kukabidhi Mwenge wa Uhuru kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni William Makufwe tayari kuukimbiza

Image may contain: one or more people and outdoor

Image may contain: one or more people and people standing

  Image may contain: one or more people, people standing and outdoor

Ufunguzi wa Bohari ndogo ya kuhifadhia Dawa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni.

Image may contain: 2 people, indoor

Baadhi ya wanafunzi wakiwa tayari kuonesha vifaa vinavyotumika kwenye maabara

Muonekano wa nje wa Maabara ya Sayansi Shule ya Sekondari Kwaluguru.

Muonekano wa ndani wa Ghala

Ufunguzi wa Ghala la Kuhifadhia mazao lililopo Kwachaga.

Wataalamu wa Afya na Madaktari wakiwa kwenye chumba cha upasuaji kituo cha Afya Mkata kuonesha wapo tayari kufanya kazi.

Baadhi ya vifaa vilivyopo kwenye jengo la Upasuaji kituo cha Afya Mkata

Mkimbiza Mwenge wa uhuru kktikati akiwa ameambatana na  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Handeni Eng Robert Gabriel Kulia na Mratibu wa Mwenge Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Kushoto Mbazi mfinanga  na wataalamu wengine mara baada ya kuweka jiwe la Msingi mradi wa tanki la kuhifadhia maji Kijiji cha Kwedikabu Kwamsisi.

Jengo la Kituo cha Afya Kwamsisi lililowekewa Jiwe la Msingi na Mwenge wa Uhuru

Mkurugenzi Mtendaji William Mkaufwe kikagua Gwaride la Halaiki

Watumishi na Watalaam mbalimbali wakiwa tayari kuupokea mwenge wa Uhuru eneo la Viwanja vya Mkesha Kwamsisi


Mkimbiza Mwenge Kitaifa Ndg.Amour Hamad Amour akikagua vifaa vya kufugia samaki vilivyotolewa kwa vikundi vya kinamama na Vijana kama Mkopo badala ya kutoa fedha Taslim.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa