• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WACHIMBAJI WADOGOWADOGO WA MADINI KATIKA KIJIJI CHA KWAMSAMPA WILAYANI HANDENI WAMEAHIDIWA KUTOKUONDOLEWA IWAPO WATAFUATA TARATIBU NA KANUNI.

Imerushwa: July 30th, 2017

Serikali Wilayani Handeni imewahakikishia wachimbaji wadogowadogo wa madini ya dhahabu zaidi ya 100 waliopo katika Kijiji cha Kwamsampa Kata ya Kwasunga kwamba hawataondolewa kwenye machimbo hayo iwapo watafuata taribu na kanuni walizowekewa.

Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Wilaya ya Handeni Godwin Gondwe Mwishoni mwa Wiki alipowatembelea wachimbaji hao na kutoa maagizo ambayo lazima wayafuate kwa usalama wao ikizingatiwa eneo hilo ni la Kijiji na hakuna Mchimbaji Mkubwa yeyote mwenye lesene ya uchimbaji wa madini katika eneo hilo.

Mkuu wa Wilaya aliwaeleza wachimbaji hao kuwa waendelee kuchimba kwenye machimbo hayo kwa kufuata taratibu za uchimbaji wa madini, wajiweke kwenye kundi  kwa kuwa na daftari la majina yao ambalo  litafuata taratibu za upatikanaji wa leseni na hatimaye kuwa na leseni halali ya wachimbaji wadogowadogo.

Gondwe Aliwataka wachimbaji hao kuacha kukata miti kiholela na badala yake wakate kwa ustaarabu ili waendelee kutunza rasilimali ya miti iliyotunzwa na wanakijiji wa eneo hilo kwa muda mrefu.Amewaeleza kuwa ni lazima wao kama wachimbaji wa Kata ya Kwasunga kutoa ushirikiano na kuheshima mamlaka ya Kijiji hicho kwa kufuata taratibu watakazopewa.

Kwa upande mwingine Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni William Makufwe amewaeleza wachimbaji hao kuwa kile kitakacho zalishwa lazima 20% iende Serikali ya Kijiji na 80% ibaki kwa wachimbaji wenyewe ili kila mmoja pate haki yake kwa utaratibu kwakuzingatia eneo ni mali ya Kijiji.

Afisa madini Mkazi Wilayani Handeni Frank Makyao ameeleza kuwa ili watambulike kama wachimbaji wa madini ni lazima waunde kikundi ambacho kitasajiliwa na kufika ofisini kwaajili ya kuwekwa kwenye mtandao ambapo itakuwa rahisi kuchukua kona nne na kupata kibali rasmi cha wachimbaji wadogowadogo.

Kamanda wa Polisi Wilayani Handeni William Nyelo amewataka wachimbaji hao kuhakikisha kuwa wanaimarisha usalama wao kwa kutoa taarifa polisi mara tu watakapoona uvunjifu wa amani ikiwa ni pamoja na kutoruhusu wageni kuingia kwenye eneo lao kiholela na kwamba watumie uhuru waliopewa na Serikali  kihalali.

  

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa