• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Wadau wa madini Handeni wafikia maazimio

Imerushwa: May 7th, 2019


Kongamano la wachimbaji wa madini Wilaya ya Handeni mkoani Tanga lililojumuisha wataalamu mbalimbali wa Halmashauri, wataalamu wa madini, Mamlaka ya mapato Tanzania, taasisi za fedha, wakala wa barabara za mijini na vijijini,wakala wa misitu, kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya pamoja na wachimbaji wenyewe limefikia maazimio baada ya kila moja kutoa changamoto zinazokabili maendeleo ya sekta hiyo Handeni.

Kongamano hilo lilifanyika tarehe 07-05-2019 katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni ambapo mgeni rasmi alikuwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Handeni Mwl. Boniphace Maiga.

Akitoa maazimio hayo Mwl. Boniphace alisema wachimbaji wa madini wanatakiwa kufuata sharia, kanuni na taratibu za uchimbaji ikiwepo kufanya tathmini ya mazingira ya maeneo ya migodi na kwamba ndani ya mwezi moja taarifa ya tathmini iwe imetolewa ofisi ya Mkuu wa Wilaya.

Azimio lingine ni uanzishwaji wa umoja wa wachimbaji madini wa Wilaya ya Handeni na amesema ndani ya siku 60 huo umoja uwe umeshaundwa kwa kuwa kupitia viongozi wa umoja huo upatikanaji wa taarifa utarahisishwa. Amesema wachimbaji au makampuni yaliyowekeza yahakikishe pia yana mikataba ya wajibu wa makampuni kwa jamii na mikataba hiyo iwasilishwe ofisi ya Mkuu wa Wilaya ili kupitishwa na pia kwaajili ya ufuatiliaji na amewaagiza hadi tarehe 17-05-2019 wawe wameshawasilisha.

Aidha amesema makubaliano yafanyike kati ya wasafirishaji na wakala wa barabara mijini na vijijini (TARURA) kuhusu matumizi ya barabara ili kuepusha malalamiko. Mwl. Boniphace ameitaka ofisi ya madini kutoa takwimu za uzalishaji wa madini za kila mwezi kwa kila Halmashauri ili ushuru wa huduma uweze kutolewa.

Pia amewataka wawekezaji na makampuni kutumia walinzi wanaotambulika au jeshi la akiba waliopewa ithibati na mkuu wa jeshi la akiba na kwamba kumtumia mtu ambaye hajapitia kwenye masuala ya ulinzi kwa taratibu zinazotambulika ni kosa kisheria na wafanyakazi wote wanaofanyakazi katika maeneo yao wachukuliwe taarifa zao kama ambavyo zinatambulika katika mamlaka mbalimbali za usajili ikiwepo anuani zao na namba za simu za ndugu zao.

Alihitimisha kwa kuwataka wachimbaji wa kati na wadogo kuhakikisha suala la ulinzi na usalama katika maeneo yao linaimarishwa pamoja na kuzingatia mpango wa matumizi bora ya ardhi ili kuepusha migogoro, wadau hao pia waliaswa kutoa elimu kwa jamii ili kutoa taarifa za wageni wanaoingia katika maeneo ya migodi.

Wadau hao kwa pamoja walikubalibaliana kufanyika kwa kongamano la wadau wa madini Handeni mara mbili kila ili kuboresha sekta hiyo Wilayani Handeni.

MWISHO.


Mgeni rasmi Mwl.Boniphace Maiga akizungumza katika kongamano la wachimbaji wa madini.

Mgeni rasmi Mwl.Boniphace Maiga akikagua madini ya Handeni yaliyokuwa yanaonyeshwa kwenye kongamano.

Wakurugenzi wa Halmashauri ya Mji (Keneth Haule wa kulia aliyeshika jiwe) na Halmashauri ya Wilaya Bw.William Makufwe kushoto wakiangalia aina za madini.

Kamati ya Ulinzi na usalama ikikagua madini

Hayo ni baadhi ya madini yanayopatikana Handeni.

Wachimbaji wa madini wakitoa changamoto zinazorudisha nyuma maendeleo ya sekta ya madini Handeni.



Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa