• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Wafugaji na Wafanyabiashara waafikiana kufufua mnada wa Mkata

Imerushwa: October 30th, 2018

WAFUGAJI NA WANAFANYABIASHARA HANDENI WAAFIKIANA KUFUFUA MNADA WA MKATA

Wafanyabiashara na wafugaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni wamekubaliana kufufua mnada wa Mkata ambao uliacha kufanya kazi tangu mwaka 2013 kutokana na sababu mbalimbali ambazo hazikuwa rafiki kwa wafanyabiashara na wafugaji hao kama vile namna ya utozaji wa ushuru, njia ya mifugo  na alama za  vivuko vya wanyama.

Maafikiano hayo yalifanyika jana katika kikao cha pamoja baina ya wadau hao na uongozi wa Halmashauri kilichofanyika katika ukumbi wa Neema ulioko Kijiji cha Mkata Mashariki ambapo kwa pamoja walikubaliana mnada kufanyika kila jumatatu kuanzia tarehe 12/11/2018

Akizungumza katika kikao hicho Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya ya Wilaya ya Handeni Bi Rahel Mbelwa aliwasihi wadau hao kushirikiana kwa pamoja na kutokujadili yaliyopita kwani kwa kipindi hicho Halmashauri zilikuwa zinatumia wazabuni ambao hawakuwa watumishi wa Serikali hivyo hawakufuata kanuni,taratibu na sheria katika ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri kwa kuwatoza watu isivyotakiwa ili kujipatia kipato kikubwa.

Aliongeza kuwa mnada wa Mkata utakuwa na faida kubwa kwa wafugaji na wafanyabiashara kwakuwa mji wa Mkata unakua na pia  unafikika kwa urahisi na kwamba wanunuzi wa mifugo watakuwa wengi  hivyo bei ya mifugo itakuwa nzuri ukilinganisha na minada mingine.

Pia alisema Mkata kuna benki ambayo itawarasishia wanunuzi na wauzaji kutotembea na fedha kwaajili ya usalama wao kwani kumekuwa na matukio ya kuporwa fedha kwa wafanyabishara kutokana na mazingira wanayofanyia kazi kutokuwa na benki na uwepo wa kituo cha Polisi Mkata utawafanya watu kufanya shughuli zao kwa usalama pia.

Naye Mkuu wa Idara ya Mifugo na Uvuvi Bw. Sekiara Kiariro alitoa ufafanuzi kuhusu mifugo ambayo haijauzwa kutozwa ushuru baada ya wafugaji kulalamika kutozwa ushuru huo, Alisema kwa kipindi hicho Halmashuri ilikuwa inatumia wazabuni ambao hawakuwa watumishi wa umma  na walitoza uhuru usiostahili ili kufikisha malengo ya Mikataba yao na kwamba huo utaratibu sasa haupo tena kwani ushuru unakusanywa na watumishi wa Halmashauri wenyewe hivyo kuwahakikshia ushuru huo kutokuwepo tena.

Pia alitoa ufafananuzi kuwa ushuru wa mfugo ni shilingi elfu tano tuu na si zaidi ya hapo mpaka hapo ambapo Serikali itatoa waraka wa mabadiliko, kwa upande vibali vya kuuza mifugo vinavyotolewa kwenye vijijini alisema ni bure hivyo wafugaji wasije wakadanganywa kuwa kuna gharama ya kukata vibali vya kuuza mifugo lakini alitoa angalizo kwa wale wafugaji ambao hawatambuliki kwenye maeneo yao wahakikishe wanatambulika kwani kwa yeyote atakayeleta mifugo yake mnadani bila kibali hatatambulika. “hii inasaidia kuzuia wizi wa mifugo na uingiaji holela wa mifugo katika maeneo yetu”alisema.

Mtendaji wa Kata ya Mkata Bw. Athumani Ndutu aliwahakikishia wafugaji kutenga njia ya mifugo kupita ili kuepuka migogoro na kwa upande wa vivuko alisema tayari alama za vivuko vya wanyama zimeshawekwa.

Kiongozi wa wafugaji Handeni Bw.Shapati kwa niaba ya wadau hao alipongeza uongozi wa Halmashauri kwa kuitisha kikao hicho na pia kufikia muafaka wa kurudisha mnada wa Mkata kwani wanaamini watauza mifugo yao kwa bei nzuri kama ilivyokuwa awail bei ambayo hawakuipata kwenye minada mingine tangu mnada huo uvunjike.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa