• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WANAFUNZI WILAYANI HANDENI WAMETAKIWA KUCHUKULIA MICHEZO SEHEMU YA AJIRA RASMI

Imerushwa: May 20th, 2017

Wanafunzi Wilayani Handeni wametakiwa kuichukulia michezo kuwa sehemu ya ajira rasmi kwa kuweka  bidii zaidi katika michezo.

Rai hiyo ilitolewa na Diwani wa Kata ya Ndolwa na  Mwenyekiti wa kamati ya huduma za jamii Mh. Joel Mabula alipokuwa akifungua kambi ya wanafunzi wanojianda na mashindano ya umoja wa michezo shule za Sekondari Tanzania (UMISSETA) yanayotarajiwa kufanyika Mkoani Tanga hivi karibuni.

 Mabula aliwaeleza wanamichezo hao kuwa michezo ni muhimu sana kwa sababu ni ajira rasmi“ Michezo kwa sasa ni ajira sio tu kwa vijana wa kiume hata wakike, na sio kwa mipira ya miguu pekee, bali  hata kwa michezo mingine kama riadha, mpira wa pete  hivyo nawashauri vijana wangu kucheza michezo hii kwa juhudi ili baadae iwasaidie” Alisema Mh. Mabula.. Alisisitiza kuwa vipaji vimekuwa vikiibuliwa katika michezo ya UMISSETA na kuendelezwa hatimaye kupatiwa ajira rasmi.

Mwenyekiti huyo aliongeza kuwa michezo ni muhimu kwa sababu inaimarisha afya ya mwili na akili. Alisema kuwa kutokanan na umuhimu huo wa michezo, vijana wamekuwa wakiimarika na kufanya vizuri katika msomo yao ya darasani kutokana na michezo kuwa na uhusiano na kufaulu katika masomo.

Mabula aliwataka wanamichezo hao vijana kuwasikiliza kwa makini walimu wao ili waweze kunufaika na elimu ya michezo waliyonayo walimu wao.Aidha, aliwataka kudumisha umoja na mshikamano ili kuweza kutwaa tunzo nyingi katika michezo hiyo.Vile vile aliahidi kuongeza mipira miwili  kwa timu  ya wavulana na wasichana  ili kuongeza kasi ya mazoezi.


“ Naomba mkawe wawakilishi wazuri wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni, mafunzo na maelekezo mnayopewa na walimu wenu  yakawaongoze vyema katika kuelekea kupata  ushindi,muige mfano wa kaka zenu Serengeti boys ambao wamefanikiwa kuwakilisha vyema Taifa kwa ushindi waliopata dhidi ya Gabon” alisema  Mabula.

Wakati huohuo Mratibu wa michezo Wilaya ya Handeni Bw. Msafiri Mhando alisema kuwa matarajia yake ni kupata ushindi kwa timu zote nne (timu ya mpira wa miguu, mpira wa pete, mpira wa wavu na riadha) wanazoziandaa kwenda kuiwakilisha Halmashuri ya Wilaya ya Handeni.


“Tunapeleka timu zetu kwenda kushindana na kila timu tunatarajia kushinda kwani tunajiandaa vizuri na hii ndio itakuwa njia nzuri ya kuitangaza Wilaya yetu ya Handeni kimichezo” alisema Bw. Msafiri.

Kambi ya Mashindano ya UMISSETA Wilayani Handeni yameanza tarehe 19/5/2017.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa