• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WANANCHI WILAYANI HANDENI WAMETAKIWA KUTUNZA VIZURI CHAKULA KWENYE MSIMU HUU WA MAVUNO

Imerushwa: June 4th, 2017

Wananchi Wilayani Handeni wametakiwa kutunza vizuri chakula katika kipindi hiki cha mavuno na kuwaepuka wafanyabiashara walaghai wanaotaka kununua mazao yao kwa bei ya chini.

 Rai hiyo ilitolewa na katibu Tawala Wilaya ya Handeni, John Mahali aliyemuwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Godwin Gondwe katika maonesho ya wakulima yaliyoandaliwa na wazalishaji wa mbegu za  SEED-CO Jana, walipotembelea shamba darasa la mahindi lililolimwa kwa kutumia mbegu za mahindi za SEED-CO kutoka kampuni ya The African Seed Company ya mjini Arusha katika Kata ya Kwamatuka Wilayani Handeni.


 Mahali aliwataka wakulima kutouza mahindi mabichi yaliyopo shambani na hata baada ya kukauka yasiuzwe yote badala yake yabaki kwa hifadhi ya chakula. “Hakikisheni wafanyabiashara wasiwalaghai kwa kuuza mahindi kwa bei ya chini, kumbukeni kuwa mtahitaji kuwa na fedha za kununulia pembejeo kwa msimu wa kilimo utakapofika. Tunzeni mahindi yenu kwenye  maghala kusubiri bei itakapokuwa nzuri ndio muuze” alisema Mahali.

 Katibu Tawala Wilaya aliwakumbusha wananchi kuwa teknolojia ya kilimo inazidi kukula kila kukicha. Aidha, aliwashauri wakulima wilaayani hapa kwenda sambamba na kasi ya teknolojia ili kujihakikishia mazao bora kwa kutumia mbegu bora zinazotoa matokeo chanya.

  “Kampuni ya African Seed wanaozalisha mbegu za mahidi za Seed-Co wana mbegu bora kama ambavyo tumeshuhudia kwenye shamba darasa muda mfupi uliopita. Ni vema wakulima mkatumia mbegu hizi kwa uhakika mkubwa wa chakula na kipato cha kutosha” alisema Mahali.

 Aidha, aliwataka wakulima kutumia mbegu kutoka kwa mawakala waliopitishwa na Wilaya ya Handeni ili kuepuka mbegu zisizo na ubora. “Chukueni mbegu kwa mawakala waliopitishwa na kamati ya pembejeo ya Wilaya na mnaponunua mbegu nunueni zenye asilimia kati ya 90-100 ndizo zenye uhakika wa kutoa mazao kwa wingi” alisema Mahali.

 Alisema wakati nchi inaelekea kuwa ya uchumi wa kati, wakulima wanawajibu wa kuongeza juhudi kwenye kilimo cha mazao ya nafaka kwa kutumia wataalamu wa kilimo waliopo ili waweze kuzalisha mazao ya kutosha kwa ajili ya kusaidia viwanda vya usindikaji nafaka na chakula. 

 Aliongeza kuwa Serikali ina mpango wa kuondoa ushuru wa pembejeo za kilimo. Alisema kuwa baada ya ushuru huo kuondolewa, bei ya pembejeo itashuka  na kuwawezesha wakulima kunufaika zaidi na kilimo. 

 Halmashauri ya Wilaya ya Handeni inatarajia kuvuna Tani 90,000 za mazao ya nafaka kwa msimu wa kilimo wa mwaka 2016/2017.


Image may contain: one or more people, people standing, cloud, sky, grass, crowd, outdoor and nature

Baadhi ya wakulima wakishuhudia shamba darasa

Image may contain: 2 people, people standing and outdoor

Wakulima wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni walionufaika na mbegu bora za mahindi za SEED-CO

Image may contain: 4 people, outdoor

Mgeni rasmi Bw. John Mahali wa kwanza kulia akipata maelekezo kutoka kwa Mtaalamu wa mbegu za SEED-CO Bw. Kassimu Nyaki.

  Image may contain: 1 person, standing, sky, grass, outdoor and nature

Baadhi ya wataalamu wa Kilimo na mbegu za SEED-CO

Image may contain: one or more people, people standing, grass, child, outdoor and nature

Mgeni rasmi Bw. John Mahali akitoka kushuhudia shamba darasa akiwa ameongozana na wakulima na wataalamu mbalimbali.

shamba darasa lililopo kwa kwamatuku.





Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HANDENI DC June 04, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa