• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WANANCHI WILAYANI HANDENI WAPATIWA ELIMU NA UHAMASISHAJI JUU YA AFYA NA HAKI YA UZAZI.

Imerushwa: October 20th, 2017

Wananchi Wilayani Handeni wamehamasishwa kujikinga na magonjwa ya ngono na ukimwi,kutokomeza ukeketaji kwa watoto wa kike, kujikinga na ujauzito na ndoa za utotoni na athari zitokanazo na kutojifungulia kwenye vituo vya afya.

 Uhamasishwaji huo umefanywa  na shirika  lisilo la kiserikali Amref Health Africa  kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Handeni kuhusu afya na haki ya uzazi.

 Akizungumza Afisa Mradi wa “Kijana wa Leo” Henry Bendera amesema kuwa lengo kuu la kufanya uhamasishaji huo ni kusaidia juhudi za Serikali za kuboresha afya na haki ya uzazi na ujinsia kwa vijana na kinamama walio katika umri wa kujifungua.

 Aliongeza kuwa mradi wa kijana wa leo unaelimisha wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni juu ya umuhimu wa kujifungulia kwenye vituo vya afya,kujikinga na magonjwa ya ngono na ukimwi, athari za ujauzito na mimba za utotoni, athari za ukeketaji na unyanyasaji wa kijinsia kwa kutumia makundi mbalimbali waliopo shuleni na nje ya shule ikiwa ni pamoja na kufanya matamasha yanayojumuisha wananchi wote.

 Mratibu wa Afya ya mama na mtoto Wilayani Handeni Bi. Neema Kombo alisema kuwa takwimu  kubwa inaonesha  wamama hawajifungulii kwenye vituo vya afya hali inayopelekea kuongezeka kwa idadi ya wamama wanaopoteza maisha kutokana na kujifungulia kwenye maeneo ambayo si salama.

 Aliongeza kuwa kuna umuhimu mkubwa wa wamama kujifungulia kwenye vituo vya afya ikiwa ni pamoja na kupatiwa huduma za wali mara tu baada ya mama kujifungua kwa usalama wake na wa mtoto, pia alisema  kuwa ni jambo la busara  mama anapojihisi kuwa ni mjamzito kwenda hospitali kuanza kliniki mapema na kupata ushauri wa daktari juu ya ukuaji wa mtoto.

 Kwa upande wake mratibu wa magonjwa ya ngono na ukimwi Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Dk. Mbonea Yonaza alitoa rai kwa wananchi ngazi ya familia kuhakikisha wanapima virusi vya ukimwi ili kuepuka maambukizi mapya ambayo mama hakuwanayo kipindi cha ujazuzito na kukinga watoto kuambukizwa.
 Aliongeza kuwa Serikali inadhamiria ifikapo 2025 kutokomeza kabisa virusi vya ukimwi ndio maana upimaji wa hiari unahamasishwa kwa wananchi wote ili asilimia 90 ya kila eneo husika wananchi wote wawe wamepimwa na kutambulika afya zao 

 Akizungumzia athari za ujauzito na ndoa za utotoni Afisa Maendeleo ya jamii Bi. Amina Waziri aliwataka wazazi kuacha tabia hiyo kwa kuwa kumuoza mtoto katika umri mdogo ni kukatisha ndoto za mtoto huyo kwani kila mtoto anandoto anazotaka kuzitimiza kupitia elimu kwa kuzingatia kuwa elimu ni haki ya msingi ya kila mtoto.

 Aliongeza kuwa ndoa za utotoni zinasababisha kuongezeka kwa watoto wanaoishi kwenye mazingira hatarishi,kuzorota kwa hali ya uchumi ngazi ya familia,mtoto kupata maradhi kama ya Ukimwi na wakati mwingine vifo wakati wa kujifungua  kwa sababu viungo vyao vya mwili vinakuwa havijakomaa kukabiliana uzazi.

 Afisa mradi msaidizi Ibrahim olekinwaa aliwaeleza wananchi athari za ukeketaji kwa watoto wa kike na kuwataka kuondokana na dhana potofu  ya kwamba mtoto wa kike aliyekeketwa hawezi kuolewa sababu hajakamilika kwa kutokukeketwa.

 Alieleza kuwa shirika la amref health Africa limeleta njia mbadala ya kusherehekea, kufanya shughuli zote za kimila  na kuvusha rika watotowa kike  kwa jamii zote za kimasai na wakulima bila kukeketa kwani kitendo hicho hakikubaliki duniani kote na kwamba ni kinyume cha haki za binadamu na ni unyanyasaji wa kijinsia.

 Mradi wa Afya na Haki ya uzazi na ujinsia wa kijana wa leo ni mradi wa miaka mitatu, ulianza kutekelezwa octoba 2015 hadi septembba 2018 na kwa awamu ya kwanza unatekelezwa kwenye kata 12 kati ya kata 21 zilizopokwenye halmashuri ya wilaya ya handeni, mradi huu unatekelezwa kwa ushirikiano wa shirika la Amref Health Africa Tanzania na Halmashauri ya Wilaya ya Handeni.

 Jumla ya kata 4 (Sindeni, Kwankonje, Kwachaga na Makata) zimehamasishwa kuhusu afya na haki ya uzazi kuanzia jumanne na kuhitimishwa ijumaa ikiwa na  takribani ya watu 300 waliojitokeza kupima kwa hiari virusi vya ukimwi



Image may contain: 2 people, crowd and outdoor

Baadhi ya wananchi waliojitokeza

Image may contain: 2 people, people standing, sky, tree and outdoor

Mratibu wa mradi kutoka Amref Bw. Henry Bendera akielimisha wananchi

  Image may contain: 11 people, people smiling, people sitting

watoa maada walioketi viti vya mbele

  Image may contain: 2 people, people smiling, people standing, crowd and outdoor

Afisa Maendeleo ya jamii Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bi. Amina Waziri akielimisha wananchi. 

Image may contain: 5 people, people smiling, people standing, crowd and outdoor

Mratibu wa Afya ya mama na mtoto Bi. Neema Kombo akielimisha wananchi.

Mratibu wa magonjwa ya ngono na ukimwi Dk .Yonaza Mbonea akielimisha wananchi.

Afisa mradi msaidizi Ibrahim Olekinwaa akielimisha wananchi madhara ya ukeketeji

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa