• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

DC HANDENI AMEWATAKA WATAALAMU NA VIONGOZI NGAZI YA KATA NA TARAFA KUSIMAMIA NA KUELIMISHA JAMII JUU YA MADHARA YA UKEKETAJI ILI KUTOMEZA KABISA VITENDO HIVYO

Imerushwa: December 7th, 2017

Watendaji na wataalamu wa Wilaya ya Handeni wametakiwa kusimamia na kuweka suala la elimu ya madhara ya ukeketaji kuwa ajenda rasmi kwenye vikao vyao  ngazi ya Kata na Tarafa ili kukomesha kabisa vitendo vya ukeketaji kwa watoto wa kike wa jamii ya wafugaji hususani pindi mradi wa “KIJANA WA LEO” unaofadhiliwa na shirika la Amref kukoma.
 .
 Mkuu wa  Wilaya ya Handeni Mh. Godwin Gondwe  ametoa rai hiyo  leo alipohudhuria sherehe za uvushwaji rika wa wasichana 170 wa jamii ya wafugaji(Ndito) zilizofanyika Kata ya Malezi katika mtaa wa Kwamadule.

 Mh. Gondwe alisema kuwa ni haki ya binti anapokuwa mtu mzima na kuvushwa rika asiweze kunyanyaswa kijinsia, kwasababu athari za ukeketaji zinafahamika ikiwa ni pamoja na kuwa ni kitendo ambacho ni kinyume na maagizo ya Mungu lakini pia uvunjwaji wa haki za binadamu..

 Ameongeza kuwa jamii ya wafugaji inatamaduni zilizoshiba na wanachangia kwa kiasi kikubwa kuingizia pato na fedha za kigeni  Taifa, ni utamaduni bora unaotambulisha Tanzania kwa zaidi ya makabila 120.Watu wanapenda tamaduni za kimasai na jamii za wafugaji wengine lakini mila ambazo ni potofu zinazoleta maumivu katika jamii zitokomezwe.

  “ sherehe na kila kitu kifanyike, watoto wafundishwe lakini ukeketaji hapana ili tumuokoe binti huyu na maumivu makali kwa sababu morani wamekubali kuoa wananwake ambao hawajakeketwa na kwasasa wanaoa hata jamii zingine ambazo wanawake hawajakeketwa” alisema Mkuu wa Wilaya.

 Aidha aliwataka wataalamu wote ngazi ya Tarafa Hadi vitongoji ikiwa ni pamoja na idara zote hususani Elimu na Mendeleo ya jamii kuendelea kutoa elimu na kubaini wale ambao bado wanaendeleza vitendo vya ukeketaji kwa siri ili kuchukua hatua za kisheria kwasababu wanakwenda kinyume na haki za binadamu na kisheria hairuhusiwi.

 
 Meneja mradi wa Amref Health Africa Dk.Aisha Byanaku amesema kuwa lengo kuu la mradi  ni kuborehsa afya ya uzazi kwa vijana ambao wako katika umri wa miaka 10-24 ambapo hadi sasa elimu kwa jamii ya wafugaji imetolewa ikiwa ni pamoja na mangariba, watoa huduma za afya na viongozi wa kimila.

 Mradi wa “KIJANA WA LEO”ulizinduliwa na Amref Health Africa Wilayani Handeni Octoba 2015 ukifadhiliwa na Allen&Overy na big Lottery fund ambapo hadi sasa jumla ya wasichana 830 wamefanyiwa sherehe za kimila (kuvushwa rika) bila kukeketwa kwa Kata za Malezi,Msomera na Kwamagome za Wilaya ya Handeni.

 Sherehe za uvushwaji rika zimehudhuriwa na wakurugenzi wa Handeni na wataalamu mbalimbali wa Halmashauri ya Mji na Wilaya ya Handeni.

Image may contain: 3 people, outdoor

Mkuu wa Wilaya ya Handeni akizungumza na jamii wa wamasai kwenye sherehe za uvushaji rika 

Image may contain: 7 people, people smiling, people standing and people on stage

Muuguzi wa kimasai akihamasisha wazazi kuwapeleka watoto shule na kuepuka ndoa za utotoni.

Image may contain: 1 person, standing and outdoor 

mmoja wa wazee wa kimila akishukuru kwa elimu iliyotolewa na Shirika la Amref Health Africa

Image may contain: 5 people

mmoja wa wsichana waliovushwa rika bila kukeketwa akipokea cheti cha kufuzu mafunzo ya kuzuia ukeketaji na mafunzo ya afya ya uzazi

Mkuu wa Wilaya ya Handeni akizungumza na Mangariba na kuwapongeza kuelimika kuacha vitendo vya ukeketaji kwa watoto wa kike

Mratibu wa mradi  kutoka Amref Health Africa Dk.Aisha Byanaku akitoa maelezo na malengo makuu ya mradi wa KIJANA WA LEO

 mangariba wakionesha namna ambavyo  huwakamata wasichana (ndito) wa kimasai kuwapeleka kwenye chumba cha ukeketaji.


wasichana wakiimba wimbo wa kupinga ukeketaji mbele ya mgeni rasmi.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa