• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WATAALAMU WA MIFUGO NA MAZAO WAMETAKIWA KUHAKIKISHA ZOEZI LA UTAMBUZI,USAJILI NA UFUATILIAJI WA MIFUGO UNAFANYIKA KWA WEREDI BILA URASIMU.

Imerushwa: October 24th, 2017

Wataalamu wa mifugo na mazao wametakiwa  kuhakikisha zoezi la utambuzi, usajili na ufuatiliaji  wa mifugo linafanyika kwa weredi na  kuacha urasimu  kwa kufuata sheria na kanuni zinazoongoza utambuzi wa mifugo.

 Rai hiyo imetolewa na Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya Bi. Upendo Magashi(Afisa Tawala) leo alipokuwa akifungua mafunzo ya wataalamu wa mifugo kuhusu sheria ya utambuzi usajili na ufuatiliaji wa mifugo , uliofanyika kwenye ukumbi wa shule ya Sekondari Handeni.

 Amesema kuwa hili ni agizo la kitaifa lenye lengo la kutambua mifugo  iliyopo kila eneo  ili kubaini idadi ya mifugo na rasilimali zinazohitajika kwenye uendelezaji wa mifugo, amesema  Ili kuweza kutambua idadi kamili ya mifugo iliyopo katika wilaya yetu  ni lazima kufanya zoezi la utambuzi usajili na ufuatiliaji wa mifugo kwa kuzingatia  sheria namba 12 ya mwaka 2010 inayohusu utambuzi,usajili na ufuatiliaji wa mifugo(livestock identification registration  na tracebility act 2010) na kanuni zake za mwaka 2011.


 Ameongeza kuwa zoezi hili ni shirikishi na wananchi wote wanapaswa kuhamasishwa na kuelimishwa ili kuondokana kabisa na kesi zinazotokana na wakulima na wafugaji waliopo kwenye Wilaya yetu; amesema kwa kufanya utambuzi wa mifugo kutasaidia kupunguza na kuondoa migogoro inayotokana wakulima na wafugaji, kutambua mifugo inayoingia wilayani kwetu kinyume na taratibu, kumwezesha mfugaji kutambua mifugo yake na kurahisisha utambuzi wake pindi mfugo unapopotea.

 Aidha amesema kuwa kutokana na sheria ya utambuzi usajili na ufuatiliaji wa mifugo kila mfugo kijijini unatakiwa kutambuliwa kwa kuwekewa chapa ya moto ambayo ni maalumu kwa kila Kijiji.utambulisho huu utasaidia kujua mifugo ambayo ni halali kwa Kijiji husika na ile amabyo ipo kijijini isivyo halali pia litaondoa tatizo la kuhamahama kwa wafugaji.

 “ yeyote atakayebainika kuwa kikwazo cha utekelezaji wa zoezi hili taarifa ifikishwe kwenye ofisi ya Mkuu wa Wilaya ili kuona ni namna gani kamati ya Ulinzi na Usalama itamshughulikia” amesema Upendo.

 Ametoa rai kwa wataalamu wa mifugo kuthamini mazao ya wakulima hususani pindi yanapovamiwa na mifugo,amesema kumekuwepo na kesi nyingi za wakulima na wafugaji juu ya uharibifu wa mazao, kila mmoja awajibike kwa nafasi yake kwani uwepo wao  kwenye ngazi ya Vijiji na Kata sio wa makosa.

 Kwaupande wake kaimu Mkurugenzi Bw. Amani Mangesho(Mwanasheria wa Halmashauri) amewataka watalamu wa mifugo na kilimo kuacha kufanya kazi kwa mazoe na kuendesha zoezi bila  ubaguzi na kuangali nani ni nani.

 Amewataka wataalamu wa mifugo kusimamia sheri inayowaongoza katika utekelezaji wa zoezi na kuhakikisha mafunzo wanayopatiwa yanawafikia wananchi juu ya umuhimu wa zoezi hili kwa kuzingatia ni agizo la kitaifa na utekelezaji wake unahitajika kwenye maeneo yote.


Image may contain: sky, cloud, tree, outdoor and nature

Baadhi ya Mifugo

Image may contain: 3 people, people sitting

Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya Bi. Upendo Magashi ( Afisa Tawala) akizungumza na Wataalamu wa Mifugo.

Image may contain: one or more people, people standing, sunglasses and stripes

Kaimu Mkuruygenzi Bw. Amani Mangesho ( Mwanasheria wa Halmashauri ) akizungumza na wataalamu wa mifugo) 

Image may contain: 4 people, people sitting

Baadhi ya Wataalamu wa Mifugo na kilimo 

Image may contain: 1 person, sitting, table and indoor








LikeShow More ReactionsCommentShare


Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa