• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WAZAZI PELEKENI WATOTO SHULENI KUEPUKA KUWA NA WATU WAZIMA WASIOJUA KUSOMA NA KUANDIKA SIKU ZA USONI

Imerushwa: October 12th, 2017

Katika kuhitimisha juma la elimu ya watu wazima wasiojua kusoma, kuhesabu na kuandika lenye kauli mbiu ya “kujua kusoma katika ulimwengiu wa sayansi na teknolojia kwa maendeleo ya nchi”mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya amewataka wazazi kuwapeleka shuleni watoto wote waliofikisha umri wa kwenda shule.

 Akizungumza kwenye Hitimisho la juma la Elimu ya Watu wazima jana  lililofanyika  Shule ya Msingi Kweditilibe  Kata ya Kiva ,Afisa Tarafa ya Sindeni Bw. Sijaona Bugufi amewaeleza wazazi umuhimu wa kuwapeleka watoto wao shuleni ili kuondokana na watu wazima wasiojua kusoma na kuandika hapo baadae.

 Aliongeza kuwa lazima tupunguze na kuondoa kabisa idadi ya watuwazima wasiojua kusoma, kuhesabu na kuandika ili kukuza uchumi wa jamii yetu na Taifa kwa ujumla, kwa maana taifa lolote lililoendelea lilianza na kuondoa ujinga miongoni mwa wananchi wake kwa kuwapa elimu.

 Alisisitiza kuwa Elimu wanayopata watu wazima isiwe ya darasani tu, lakini pia ijikite kwenye ujasiliamali ili wazee wetu wajishughulishe katika shughuli mbalimbali zitakazowaongezea kipato na kujenga uchumi wa taifa letu kwani ndani ya hizo shughuli ndogondogo ndipo kunapopatikana na viwanda vidogovidogo katika kuelekea uchumi wa viwanda.

 Aliwaasa wananchi kushiriki kikamilifu kwenye shughuli za maendeleo ya maeneo yao ikiwa ni pamoja na kujitolea  nguvu kazi kwenye ujenzi wa miundo mbinu iliyopo kwaajili ya manufaa ya vizazi vyao, ikiwa ni pamoja na Maabara, madarasa na nyumba za walimu.
 “katika kupeleka gurudumu la maendeleo mbele lazima wote tushiriki nguvu kazi, natoa rai kwa wananchi maabara zilizoanzwa kujengwa zimaliziwe ili watoto wetu waweze kujifunza kwa vitendo  na kuongeza ufaulu wa  masomo yote ya sayansi” Alisema Bugufi.

 Mwisho aliwaeleza wananchi kuwa changamoto zote zilizoanishwa kwenye Risala yao amezipokea na atazifikisha ofisini kwa Mkuu wa wilaya ili kuona ni namna gani ambavyo wanaweza kushirikiana kuzitatua kwa pamoja na kumtaka Mkuu wa Shule ya Msingi Kobil kuandika barua inayoainisha changamoto wanazokabiliana nazo na kufikisha  ofisi ya Mkuu wa Wilaya.

 Kwaupande wake Kaimu Mkurugenzi Bi. Nipael Ezekieli (Mwanasheria wa Halmashauri) aliwasisitiza watoto kusoma kwa bidii na kutumia fursa ya elimu bure  ambayo Serikali inagharamia kwa kiasi kikubwa kuhakikisha wananchi wake wote wanapata elimu za Msingi.

 Katika kupambana na mapambano dhidi ya wasiojua kusoma na kuandika Halmashauri ya Wilaya ya Handeni imeweza kuendesha madarasa 10 ya MEMKWA yenye wananfunzi wapatao 489 kati yao wavulana 312 wasichjana 177 na uwepo wa idadi hii umetokana na wanafunzi walioacha shule kwasababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na umbali wa shule, kuhamahama kwa wazazi na utayari duni wa wazazi kufuatilia maendeleo ya watoto wao hali inayopelekea watoto hao kuacha shule na idadi ya wasiojua kusoma na kuandika  kuongezeka .

 Elimu inayotolewa kwa watuwazima mbali na kujua kusoma, kuhesabu na kuandika, elimu ya ujasiliamali, vikoba,kilimo na vikundi mbali mbali inatolewa ili kuwakwamua kichumi.
 Juma la elimu ya watu wazima limeadhimishwa kuanzia tarehe  5-12 octoba 2017 badala ya tarehe 1-8 septemba  sababu za kupelekwa mbele ni kufanyika kwa mitihani ya taifa ya darasa la saba na shughuli za mapokezi ya  Mwenge wa Uhuru.

 Juma hilo limehudhuriwa na Viongozi mbalimbali kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Handeni huku mgeni rasmi akiwa ni Bw.Sijaona Bugufi afisa Tarafa ya Sindeni akimuwakilisha Mkuu wa Wilaya Mh. Godwin Gondwe aliyekuwa na majukumu mengine.



Image may contain: 16 people, people sitting

Baadhi ya walengwa wa elimu ya watu wazima

Image may contain: 27 people, people smiling, crowd

Wanafunzi na wananchi walioshiriki kwenye maadhimisho hayo

  Image may contain: 4 people, people sitting and indoor

Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya Bw. Sijaona Bugufi (Afisa Tarafa Sindeni) Akizungumza na wananchi kwenye maadhimisho

Image may contain: 1 person, standing and outdoor

Wanafunzi shule ya Msingi Kweditilibe wakiongoza wimbo wa Taifa

  Image may contain: 6 people, people standing and indoor

Viongozi wakiimba wimbo wa Taifa

Mh.Diwani Kata ya Kiva  Rajabu Kibwana akizungumza kama Diwani wa Kata, Mwenyekiti wa Halmashauri na Mwenyekiti wa Hufuma za jamii

Mkuu wa Idara ya Elimu Msingi Bw. Fikeni Senzighe akizungumza kwenye maadhimisho hayo.

Afisa Elimu ya Watu wazima Bw. Elibariki Mfinanga akizungumza kwenye maadhimisho hayo.

Kaimu Mkurugenzi Bi. Nipael Ezekiel( mwanasheria wa Halmashauri) akizungumza kwenye maadhimisho hayo













Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa