• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Waziri Mkuu Majaliwa afanya ziara ya kikazi Handeni

Imerushwa: March 4th, 2020


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Kasim Mjaliwa Majaliwa alifanya ziara ya kikazi Wilayani Handeni Mkoani Tanga jana, lengo likiwa ni kuona utekelezaji wa shughuli za seriikali pamoja na kusikiliza na kutatua kero za wananchi.

Mh. Majaliwa alizungumza na wananchi wa Handeni katika miji midogo ya Michungwani, Kabuku, Mkata na viwanja vya shule msingi Chanika.

Akijibu kero za wananchi ikiwepo uhaba wa vituo vya afya na wataalamu wa afya, uhaba wa maji safi na salama, wawekezaji kumiliki mashamba makubwa bila kuziendeleza, barabara mbovu na ukosefu wa umeme katika baadhi ya vijiji alisema serikali ipo kwaajili ya kuhudumia wananchi hivyo itatatua kero hizo kwa wakati ili waweze kuishi maisha bora.

Kwa upande wa vituo vya afya alisema serikali tayari imeshaanza kupeleka fedha katika Halmashauri ili kupunguza adha ya Hospitali za Wilaya kulemewa na alisema mwaka huu serikali itatoa ajira ya madaktari hivyo aliwatoa hofu wananchi kuwa madaktari Handeni wataletwa lakini kwa upande wa Zahanati aliwahimiza wananchi kuanzisha ujenzi wa majengo ya Zahanati na kuzielekeza Halmashauri kupitia mapato ya ndani kumalizia majengo hayo ili wananchi wweze kupata huduma karibu na maeneo yao wanayoishi.

Waziri Majaliwa alisema serikali pia imeshatoa fedha kwaajili ya ukarabati wa barabara lakini kutokana na mvua nyingi zinazoendelea kunyesha hazitaweza kukarabatiwa lakini baada ya msimu wa mvua kuisha barabara zote zitakarabatiwa isipokuwa zile barabara zilizokata mawasiliano zinatakiwa zitengenezwe baada tu ya kuharibika bila kusubiri msimu wa mvua kuisha. Kwa suala la umeme amesema serikali iko kwenye mkakati wa kusambaza umeme katika vijiji na vitongoji vyote nchi nzima hivyo wananchi wawe na subira watafikiwa na kwamba umeme huo mwananchi ataunganishiwa kwa Sh. 27000 tu na nguzo atawekea bure hata kama umbali wa kufika nyumbani utahitaji nguzo zaidi ya moja.

Aidha aliwataka wawekezaji waliochukua maeneo makubwa bila kuziendeleza kunyang’anywa na kurudishiwa wananchi ili waendelee na shughuli za uzalishaji na kwamba wale waliopewa maeneo na vijiji zaidi ya ekari 50 warudishe kwakuwa vijiji havina mamlaka ya kutoa maeneo zaidi ya ekari hamsini. Pia akizungumzia suala la maji Mh. Majaliwa alisema serikali inalifanyia kazi na kuzielekeza mamlaka za maji kuhakikisha wananchi wanapata maji ambayo ni salama na kuwaeekeza kubaini maeneo ya kuchimba visima vya maji ili wananchi waondokane na adha hiyo kutekeleza kampeni ya Mh. Raisi ya kumtua mama ndoo.

Alihitimisha kwa kuwataka watumishi wa umma kuhakikisha wanawatumikia wananchi kwa weledi na kwamba wanatakiwa kwenda vijijini kutatua kesho za wananchi badala ya kukaa maofisini  siyo mpaka kiongozi wa serikali aje ndipo walete kero zao hususani kupitia mabango.

Katika ziara hiyo Waziri Mkuu pia alitembelea kiwanda cha kutengeneza unga wa mahindi kilichopo Kata ya Mkata Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Mkoani Tanga.

MWISHO.


Imeandaliwa na;

Paulina John

Kitengo cha Habari na mawasiliano Handeni DC.

Waziri Mkuu Mh. Kasim Majaliwa akizungumza na wananchi na wananchi wakimsikiliza

Waziri Mkuu Mh.Kasim Majaliwa akizungumza jambo na mwekezaji wa kiwanda cha kutengeneza unga wa mahindi baada ya kukagua

Mh. Waziri Mkuu Kasim Majaliwa akisilikiza maelezo ya mwekezaji wa kiwanda cha kutengeza unga wa mahindi Mhandisi Mwambashi wa kushoto 

Waziri wa madini Mh.Doto Biteko akisalimia wananchi

Naibu Waziri wa maji Mh.Jumaa Aweso akiwatoa hofu wananchi kwa kutatua kero ya uhaba wa maji safi na salama maji

Naibu Waziri wa kilimo Mh.Omary Mgumba akisalimia wananchi

Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mh.Martin Shigela akisema neno la ukaribisho wa Waziri Mkuu Wilayani Handeni

Mbunge wa Handeni Vijijini Mh.Mboni Mhita akiwasilisha changamoto za Handeni kwa Mh.Waziri Mkuu

Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh.Godwin Gondwe akijibu maswali ya Mh.Waziri Mkuu

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bw. William Makufwe akijibu maswali ya Mh.Waziri Mkuu

Wakurugenzi wa Handeni vijijini Bw. William Makufwe kushoto na Handeni Mji  Bw.Keneth Haule kulia wakimskiliza Mh.Waziri Mkuu 

Viongozi mbalimbali wakifuatilia mazungumzo ya Mh. Waziri Mkuu

Afisa Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji Bi. Edina Katalaiya wa kwanza kulia akipokea maagizo kutoka kwa Mh.Waziri Mkuu

Watumishi mbalimbali wakifuatilia hotuba ya Mh.Waziri Mkuu

Wananchi wakitoa kero zao kwa Mh.Waziri Mkuu


Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa