• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

HALMASHAURI YA WILAYA YA HANDENI YAPOKEA MICHE 4000 YA MBEGU ZA MIKOROSHO.

Imerushwa: April 27th, 2017

Halmashauri ya Wilaya ya Handeni imepokea miche 4000 ya mbegu za korosho kutoka bodi ya korosho ili  kuunga mkono juhudi za Serikali ya Halmashauri ya Wilaya ya Handeni ya kuanzisha korosho kama zao la biashara.

Miche hiyo ya mbegu za Mikorosho zilipokelewa na Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh. Godwin Gondwe na kukabidhiwa kwa Maafisa Elimu tayari kupelekwa kwenye Shule zao kwa ajili ya kwenda kupanda.

Akizungumza na Maafisa Ugani, Wakuu wa Shule za Msingi na Sekondari na Maafisa Kilimo Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh. Gondwe alieleza kuwa, kwa  muda mrefu Halmashauri ya Wilaya ya Handeni imekuwa haina zao la biashara la uhakika na wakati huohuo kuna ukanda ambao unakubali kustawi kwa zao la korosho, hivyo ni muhimu kuchukulia zao hili kama zao la biashara bila kujali ni muda gani unachukua mpaka mavuno.

“korosho linakuwa ni zao la biashara  Wilayani Handeni, ni mti ambao utasaidia kutunza mazingira pia, lengo ni kuongeza uchumi wa wananchi, kushirikisha wanafunzi kwenye elimu ya kujitegemea na kuhakikisha wanafunzi hawapati shida ya chakula hatimaye kuongeza kiwango cha uelewa na ufaulu kwa watoto wetu” alisema Mh. Gondwe.

Mh.Gondwe Aliongeza kuwa mbegu hizi zitasambazwa kwenye taasisi za elimu hasa kwa shule ambazo zipo ukanda  wa korosho na hazikupata mbegu za mihogo au zilipata kwa kiwango kidogo, ili iwe rahisi kusimamia na kufanya mashamba darasa kwa jamii inayozunguka shule.

Mh. Gondwe Aliwataka Maafisa kilimo kuwaandikia barua zitakazowataka  kusimamia na kutoa elimu ya kilimo bora cha zao la mikorosho maafisa ugani wote watakaohusika na upokeaji wa mbegu kwenye maeneo yao.

Kuhusu suala la masoko Mh. Gondwe aliwatoa hofu na kuwaeleza kuwa masoko ya korosho Tanzania yapo na bado ataendelea kutafuta masoko huku akiwaasa katika suala la  uvunaji  bora ambao utaanzia kwenye matunzo ya zao  tangu kupandwa hadi kuvunwa.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Mh. Ramadhani Diliwa aliwaeleza wanachi kuwa wananchi wa Wilaya ya Handeni hawajachelewa kuanza zao hilo na kulima mazao mengine ya biashara huku akisisitiza upandaji wa miti ambao kwa wakati mwingine ni kutunza mazingira na kwa upande mwingine ni biashara.

“ Tuache kushikilia zao la mahindi kama zao kuu la Handeni, wananchi amkeni, limeni mazao mengine ardhi ya Handeni inarutuba ya kutosha na uwezo wa kustawi mazao mengine zaidi ya mahindi, mimi nina ekari zaidi ya 50 ambazo nimelima mazao mbalimbali na kupanda miti aina tofauti karibuni mje kujifunza ” alisema mwenyekiti.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Bw. Simon Mdaki alishukuru kupokea mbegu hizo na kuwataka Maafisa Kilimo, Wakuu wa Shule kusimamia ukuaji wa zao hilo kwa weledi ili kuweza kufikia lengo la  Halmashauri ya Wilaya ya Handeni katika kuondoa dhana potofu ya wananchi wa Wilaya ya Handeni kutegemea zao moja tu la mahindi.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa