• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Wilaya ya Handeni yapokea vitambulisho awamu ya pili

Imerushwa: February 3rd, 2019

WILAYA YA HANDENI  YAPOKEA VITAMBULISHO VYA AWAMU YA PILI.

Wilaya ya Handeni imepokea vitambulisho  vya awamu ya pili ambapo imepokea vitambulisho 5000 na kugawiwa jana katika Shule ya Sekondari Handeni kwa Maafisa Watendaji wa Kata zote za Wilaya Handeni  ili viwafikie wajasiriamali wadogo katika maeneo yote ya Wilaya Handeni.

Akizungumza katika kikao cha maelekezo ya kusimamia uuzwaji wa vitambulisho hivyo Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh. Godwin Gondwe ambaye alikuwa mgeni rasmi aliwapongeza Watendaji hao kwa kufanya vizuri katika uuzaji wa vitambulisho awamu ya kwanza na kuwasihi kuongeza juhudi zaidi  awamu hii ya pili kwa kumaliza kwa wakati.

Gondwe amewaasa watendaji kuhakikisha wafanyabiashara ambao hawalipi kodi wote wanapata  vitambulisho na kusiwe na urasimu wa kugawa vitambulisho hivyo kwa kigezo cha mtu kukosa viambata vya kupata kitambulisho hivyo mtu akiwa na fedha apewe kitambulisho chake viambata apeleke baadaye na kwamba baada ya kutoa kitambulisho watendaji hao wahakikishe wanaweka kumbukumbu ya uuzwaji wa vitambulisho vizuri .

Aidha aliwataka Watendaji kuelimisha wafanyabiashara kwa kushirikiana na wataalamu walioko ngazi ya Kata baada ya kukaa kikao cha Kata juu ya unafuu wa kuchukua kitambulisho badala ya kutoa vitambulisho hivyo bila wafanyabiashara kutokuwa na uelewa wa kutosha wa matumizi ya vitambulisho hivyo.

Pia aliwaeleza Watendaji hao kutoa taarifa pale wanapokutana changamoto kwa uongozi ili kutatua haraka iwezekanavyo na kwamba kila ijumaa ya wiki watoe taarifa ya uuzwaji wa vitambulisho na hadi kufika tarehe 28/02/2019 vitambulisho vyote viwe vimeshauzwa.

Wakati huo huo Mh. Gondwe aliwataka Wakurugenzi kuwaandikia barua ya kuwaachisha kazi Watendaji  wanaojitolea na kuwakaimisha watumishi wa Serikali ngazi Kata wakimemo Maafisa Ugani na mifugo kwani Watendaji wakujitolea wamekuwa wakitafuta maslahi yao binafsi badala ya kuitumikia Serikali.

Alihitimisha kwa kuwataka Watendaji kuweka masuala ya kilimo, Elimu, miradi ya Maendeleo na Vitambulisho kuwa agenda ya kudumu katika vikao vya Kata.

Katibu Tawala wa Wilaya ya Handeni Mwl. Boniphace Maiga aliwataka Watendaji kufanya kazi kwa weledi na kuepuka rushwa kwani baadhi yao wamekuwa wakijihusisha na masuala ya rushwa na alisema endapo mtu atagundulika atachukuliwa hatua stahiki. Pia aliwataka  watendaji kushirikiana kupekua miradi ya maendeleo iliyoko kwenye maeneo yao kwani kuna baadhi ya maeneo hawajui miradi iliyoko katika maeneo yao zaidi ya mtu aliyeko kwenye kituo cha mradi na kwamba jambo lolote likitokea ngazi ya Kata uongozi wa Wilaya ujulishwe mapema ili kurahisisha ufuatiliaji.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bw. William Makufwe alisema lengo la Mh. Raisi ni kuwajengea watanzania utamaduni wa kulipa kodi na tozo mbalimbali ambazo zipo kwa mujibu wa sheria ili kuondokana na utegemezi wa wafadhili kutoka nje na pia kupata takwimu ya wafanya biashara na aina za biashara pamoja na kuondoa ushuru ambao wanatozwa wafanyabiashara bila kufuata kanuni na sheria.

Pia aliwataka Watendaji hao kuwa na utamaduni wa kutekeleza maelekezo badala ya kulalamika au kupuuza kwani mara nyingi wakipewa maelekezo wamekuwa wakipuuza.

Aidha aliwataka Watendaji hao kuwafuata wajasiriamali waliko badala ya kuwasubiri maofisini ili kurahisisha ufanikishaji wa zoezi hilo na alitaja wajasiriamali wanaotakiwa kupewa vitambulisho ambao ni watu wenye mapato ghafi isiyozidi milioni nne kwa mwaka, ambao hawana TIN namba na ambao wana TIN namba lakini hawajalipa kodi kwa muda mrefu.

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Handeni Bw. Keneth Haule alisema kuwa jambo lolote linaloamuliwa na mamlaka halali ni sheria hivyo aliwataka watendaji Kata washirikiane na viongozi wa ngazi ya Kata ili kukamilisha majukumu kwa pamoja na kwamba wasifanye kazi kwa udungu na mazoea bila kufuata sheria.

Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania wa Handeni Bw. Kamuhanda alisema kuwa ofisi yake iko tayari kushirikiana uongozi wa Wilaya ili kufanikisha zoezi la uuzwaji wa vitambulisho lakini aliwaasa watendaji kutokuwalazimisha wafanyabiashara wenye leseni kuchukua vitambulisho kwani inaweza kuleta mkanganyiko wa taarifa za wafanyabiashara hao.

Watendaji wa Kata kwa pamoja waliafiki kufanya kazi kwa weledi na kwa moyo ili  kufikia azma ya  Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.

MWISHOO.

Mkurugenzi Mtendaji Handeni DC Bw. William Makufwe akitoa maelekezo

Mkurugenzi Mtendaji Handeni Mji Bw. Keneth Haule akitoa nasaha.

Katibu Tawala Wilaya Mwl.Boniphace Maiga akitoa neno la Ushauri kwa Watendaji Kata

Wajumbe wa kikao wakiomba kwaajili ya Afisa biashara (Charles) aliyepata ajali katika ugawaji wa vitambulisho vya awamu ya kwanza.



Watendaji Kata wakipokea Vitambulisho na kusaini kukiri kupokea vitambulisho hivyo


Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa